Kisha nikasikia sauti ingine kutoka mbinguni ikisema: “Mutoke katika muji ule ninyi watu wangu, kusudi musishiriki zambi zake na kupatwa vilevile na mapigo yatakayoupata.
Kwa maana Mungu anasema hivi katika Maandiko Matakatifu: “Kwa wakati uliofaa, nilijibu maombi yako. Kwa siku ya wokovu, nilikusaidia.” Basi sasa, huu ndio wakati unaofaa, sasa leo ni siku ya wokovu.
Walipowatosha inje ya muji, malaika mumoja wao akawaambia: “Mukimbie kwa ajili ya usalama wenu. Musiangalie nyuma wala kusimama popote katika bonde. Mukimbilie kwenye milima, musipate kuangamia.”
Basi, Loti akawaendea wachumba wa wabinti zake, akawaambia: “Haraka! Mutoke pahali hapa, maana Yawe atauangamiza muji huu.” Lakini wao wakamwona kama mutu mwenye kuchekesha tu.
Loti akakuwa anasitasita. Lakini kwa vile Yawe alivyomuhurumia Loti, wale wamalaika wakamushika yeye, muke wake na wabinti zake wawili, wakamutosha inje ya muji.