Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 18:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Halafu Abrahamu akachukua siagi, maziwa na ile nyama uliotayarishwa, akawatayarishia wageni hao chakula; naye akasimama karibu nao walipokuwa wakikula chini ya muti.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 18:8
17 Referans Kwoze  

Loti akawasihi sana, kwa mwisho wakakubali, wakageuka na kuingia katika nyumba yake. Loti akatayarisha karamu, akachoma mikate isiyotiwa chachu, wakakula.


Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami.


Wandugu, ninyi muliitwa na Mungu kusudi mukuwe watu huru. Basi musitumie uhuru huu kuwa ruhusa ya kutimiza tamaa za mwili, lakini musaidiane kwa upendo.


Hakuonekana kwa watu wote, lakini kwa sisi tuliochaguliwa na Mungu kuwa washuhuda. Ni sisi tuliokula na kunywa pamoja naye nyuma ya kufufuka kwake.


Kule wakamutayarishia chakula cha magaribi. Marta aliwashugulikia, na Lazaro alikuwa mumoja wa wale waliokula pamoja na Yesu.


Akakitwaa na kukikula mbele yao.


Alipokuwa akiikaa kula chakula pamoja nao, akatwaa mukate na kuubariki. Kisha akaumega na kuwapatia.


Si vile, yeye atamwambia kwanza amupigie chakula na kujitayarisha vizuri kusudi amushugulikie mpaka atakapomaliza kula na kunywa. Kisha pale, ataweza kula na kunywa.


Heri watumishi wale bwana wao atakaowakuta wakikesha wakati anapofika! Kweli ninawaambia: atafunga mukaba wake vizuri na kuwakaribisha kula chakula, na kubakia pale akiwashugulikia.


Wakati ule wakachagua watu wa kuchunga vyumba vya gala ambamo matoleo kwa ajili ya hekalu yaliwekwa, malimbuko ya kwanza, zaka na kuyakusanya kutoka katika mashamba ya miji, kwa ajili ya makuhani na Walawi kama ilivyotakiwa na Sheria. Watu wote wakafurahia makuhani na Walawi waliotumika,


Manoa akamwambia huyo malaika wa Yawe: “Tafazali, ukae kidogo tukutayarishie mwana-mbuzi.”


Sisera alimwomba maji, naye akamupa maziwa; akamuletea siagi katika bakuli ya heshima.


Aliwapa siagi na maziwa ya mifugo, mafuta ya wana-kondoo na kondoo dume, makundi ya mifugo ya Basani na mbuzi. Aliwapa ngano nzuri kabisa na divai mupya wakakunywa.


Kisha akatoka haraka akakwenda kwenye kundi la ngombe, akachagua mwana-ngombe mumoja muzuri na munono, akamupatia mutumishi ambaye aliharakisha kumuchinja na kumupika.


Wale wageni wakamwuliza: “Muke wako Sara yuko wapi?” Abrahamu akawajibu: “Yuko ndani ya hema.”


Atakula maziwa na asali mpaka atakapojua kukataa mabaya na kuchagua mema.


nao watatoa maziwa kwa wingi hata aweze kula siagi. Watu watakaobaki katika inchi watakula maziwa na asali.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite