Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 18:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kisha akatoka haraka akakwenda kwenye kundi la ngombe, akachagua mwana-ngombe mumoja muzuri na munono, akamupatia mutumishi ambaye aliharakisha kumuchinja na kumupika.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 18:7
11 Referans Kwoze  

Lakini mwana wako huyu aliyeharibu mali yako katika ukahaba alipofika, ukamuchinjia yule ngombe mwenye kunona!’


Mutumishi ule akamujibu: ‘Mudogo wako amerudia salama; kwa hiyo baba yako amechinja yule ngombe mwenye kunona.’


Kisha, mulete yule ngombe mwenye kunona na kumuchinja; nasi tutakula na kufurahi pamoja.


Kisha akawatuma watumishi wengine, akisema: ‘Mwende kuwaambia waalikwa kwamba karamu yangu iko sasa tayari. Nimechinja ngombe na nyama wenye kunona; vitu vyote viko tayari. Muwaambie wafike kwa karamu!’


Alaaniwe mutu yeyote anayenidanganya, ambaye anaahidi kwa kiapo kunitolea sadaka ya nyama safi kutoka kundi lake, lakini ananitolea sadaka ya nyama mwenye kilema. Mimi ni mufalme mukubwa, na watu wa mataifa yote wananiogopa. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Ole kwenu ninyi munaolalia juu ya vitanda vya pembe za tembo na kujinyoosha juu ya matandiko yao, mukikula nyama za wana-kondoo na wana-ngombe!


Loti akawasihi sana, kwa mwisho wakakubali, wakageuka na kuingia katika nyumba yake. Loti akatayarisha karamu, akachoma mikate isiyotiwa chachu, wakakula.


Abrahamu akarudi haraka ndani ya hema akamwambia Sara: “Tayarisha haraka vipimo vitatu vya unga bora, uuponde, uchome mikate.”


Halafu Abrahamu akachukua siagi, maziwa na ile nyama uliotayarishwa, akawatayarishia wageni hao chakula; naye akasimama karibu nao walipokuwa wakikula chini ya muti.


Yule mwanamuke alikuwa na mwana-ngombe wake mumoja katika nyumba yake aliyenona, akamuchinja haraka, akatwaa unga wa ngano, akauponda, akatengeneza mukate usiotiwa chachu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite