Hapo Abrahamu akainama uso mpaka chini, akacheka ndani ya moyo wake akiwaza: “Itawezekana kweli mutoto kuzaliwa kwa muzee wa miaka mia moja? Na namna gani, Sara ambaye umri wake ni miaka makumi tisa, ataweza kupata mutoto?”
Asubui, yule mwanamuke akakuja mpaka kwenye mulango wa nyumba ambamo bwana wake alikuwa, akaanguka chini pale kwenye mulango na kubakia pale mpaka kulipopambazuka kabisa.
Elisha akamwambia: “Mwaka kesho, kwa wakati kama huu, utakuwa na mutoto katika mikono yako.” Mama akamujibu: “Hapana, Bwana wangu! Wewe ni mutu wa Mungu; usinidanganye mimi mutumishi wako!”