Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 18:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe alimutokea Abrahamu kwenye miti ya mielo ya Mamure. Abrahamu alikuwa anaikaa kwenye mulango wa hema yake wakati wa joto la muchana.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 18:1
17 Referans Kwoze  

Mutu mumoja aliyeponyoka, akakwenda kumwarifu Abramu Mwebrania ambaye alikuwa anaishi karibu na mielo ya Mamure Mwamori. Mamure alikuwa ndugu ya Eskoli na Aneri. Wote walikuwa wamefanya agano na Abramu.


Kwa hiyo, Abramu akaongoa hema, akakwenda kukaa karibu na mielo ya Mamure kule Hebroni. Kule akajengea Yawe mazabahu.


Yakobo akamwambia Yosefu: “Mungu Mwenye Nguvu alinitokea nilipokuwa kule Luzu katika inchi ya Kanana, akanibariki.


Yawe akamutokea Isaka na kumwambia: “Usiende Misri, lakini ukae katika inchi nitakayokuambia.


Stefano akamujibu: “Wandugu zangu na wababa zangu, munisikilize! Mungu mwenye utukufu alimutokea babu yetu mukubwa Abrahamu wakati alipokuwa angali katika inchi ya Mesopotamia, mbele hajahamia katika muji Harani.


Usiku ule, Mungu akamutokea Solomono, akamwambia: “Omba kitu chochote unachotaka, nami nitakupa.”


Basi, Mungu alipomaliza kuongea, akamwacha Abrahamu.


Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea.


Musa akamwambia Mungu: “Lakini Waisraeli hawataniamini wala kunisikiliza. Watasema kwamba wewe Yawe haukunitokea.”


Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.


Musisahau kuwakaribisha wageni, maana kwa kufanya hivi wamoja wamewakaribisha wamalaika pasipo kujua.


Kutoka pale, wale watu wakashika njia kuelekea Sodoma, lakini Yawe akabaki, akisimama pamoja na Abrahamu.


Abrahamu alisafiri toka kule na kuelekea eneo la Negebu, akafanya makao yake kati ya Kadesi na Suri, kisha akakwenda kukaa kwa muda kule Gerari.


Yakobo akaondoka akakwenda Mamure kwa baba yake Isaka, kule Kiriati-Arba ni kusema Hebroni, pahali ambapo Abrahamu na Isaka walikaa kama wageni.


Siku moja Yoshua alipokuwa karibu na muji wa Yeriko, aliona kwa rafla mutu mumoja akisimama mbele yake na upanga uliochomolewa katika mukono wake. Yoshua akamwendea, akamwuliza: “Wewe ni wetu au ni wa waadui zetu?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite