Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 16:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Malaika akamwuliza: “Hagari, mujakazi wa Sarai! Unatoka wapi na unakwenda wapi?” Hagari akamujibu: “Ninamukimbia bibi mukubwa wangu Sarai.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 16:8
15 Referans Kwoze  

Lakini Yawe Mungu akamwita yule mwanaume: “Uko wapi?”


Yawe akasema: “Umefanya nini? Damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika udongo.


Mutawala akikukasirikia, usiache kazi; makosa makubwa yanaweza kufutwa ukiwa munyenyekevu.


Basi, sasa bwana wangu mufalme, usikie maneno ya mutumishi wako. Ikiwa Yawe ndiye aliyekuchochea ukuje kunishambulia, basi, apokee sadaka ambayo itamusukuma kubadilisha mawazo yake. Lakini ikiwa ni watu, basi, Yawe awalaani watu hao maana wamenifukuza kutoka urizi ambao Yawe aliotupa wakisema: ‘Kwenda uitumikie miungu mingine.’


Abramu akatwaa Hagari, naye Hagari akapata mimba. Lakini mara tu alipoona amepata mimba, Hagari akaanza kumuzarau bibi mukubwa wake.


Basi, Sarai, muke wa Abramu, alikuwa bado hajamuzalia mutoto, naye alikuwa na mujakazi aliyeitwa Hagari, kutoka Misri.


Yule malaika wa Yawe akamwambia: “Rudi kwa bibi mukubwa wako Sarai na umutii.”


Kule, akafika kwenye pango, akakaa mule. Mara moja Yawe akamutolea ujumbe: “Elia! Unafanya nini hapa?”


Basi, Elia aliposikia sauti hiyo, alijifunika uso kwa koti lake, akatoka na kusimama kwenye mulango wa pango. Halafu, akasikia sauti: “Elia! Unafanya nini hapa?”


Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.


Muzee yule alipoangalia na kumwona yule musafiri akiwa kule katika kiwanja, akamwuliza: “Umetoka wapi na unakwenda wapi?”


Halafu Gehazi akaingia kwa Elisha na kuanza kumutumikia. Elisha akamwuliza: “Unatoka wapi?” Gehazi akajibu: “Sikuenda nafasi yoyote.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite