Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 16:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Abramu akatwaa Hagari, naye Hagari akapata mimba. Lakini mara tu alipoona amepata mimba, Hagari akaanza kumuzarau bibi mukubwa wake.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 16:4
11 Referans Kwoze  

mwanamuke asiyependwa anayeolewa; na mujakazi anapotwaa nafasi ya bibi yake.


Wandugu zangu, nimesema maneno haya nikitwaa mufano wa Apolo na wangu mimi mwenyewe kusudi yakuwe fundisho kwenu. Nilitaka kwamba kufuatana na mufano huu mujifunze maana ya masemi haya: “Musipite pembeni ya maandiko.” Hata mutu mumoja kati yenu asijivunie mutu fulani na kuzarau mwingine.


Sanduku la Yawe lilipokuwa linaingia katika muji wa Daudi, Mikali binti wa Saulo alichungulia kwenye dirisha, akamwona mufalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele ya Yawe. Basi, akamuzarau ndani ya moyo wake.


Kisha, Sarai akamupa Abramu Hagari, mujakazi wake Mumisri, akuwe muke wake. Haya yalitokea nyuma ya Abramu kukaa katika inchi ya Kanana kwa muda wa miaka kumi.


Sarai akamwambia Abramu: “Lazima ya ubaya ninaotendewa ikuwe juu yako. Mimi nilikupa mujakazi wangu, lakini alipopata mimba, mimi nimekuwa kitu bure mbele ya macho yake! Yawe ahukumu kati yako na mimi!”


Wakiwa kule, binti mukubwa akamwambia dada yake: “Baba yetu ni muzee na hakuna mwanaume katika inchi wa kutuoa tupate watoto.


Siku moja Sara akamwona Isimaeli, mutoto wa Abrahamu aliyezaliwa na Hagari Mumisri, akicheza na Isaka mwana wake.


Kwa hiyo Rakeli akamupa Yakobo mujakazi wake, Biliha akuwe muke wake, naye akalala naye.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite