Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 15:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yawe akamwambia: “Uniletee ngombe dike wa miaka mitatu, mwana-mbuzi dike wa miaka mitatu, kondoo dume wa miaka mitatu, na hua na kitoto cha njiwa.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 15:9
18 Referans Kwoze  

Wakatoa vilevile sadaka sawa vile inavyoagizwa katika Sheria ile: “Hua wawili au vitoto viwili vya njiwa.”


Kisha kuhani atatwaa mumoja wa wale hua au njiwa wawili kadiri mutu yule anavyoweza kuleta.


Ataleta vilevile hua wawili au vitoto viwili vya njiwa kadiri anavyoweza mumoja atakuwa kwa ajili ya sadaka ya zambi na mwingine kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa.


Musa akamwambia Haruni: Twaa mwana-ngombe dume kwa ajili ya sadaka ya kuondoa zambi na kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, nyama wote wasikuwe na kilema. Kisha uwatoe sadaka mbele ya Yawe.


Kama sadaka hiyo ya amani unayomutolea Yawe ni kutoka kundi la kondoo au mbuzi, basi achaguliwe dume au dike asiyekuwa na kilema.


Kama mutu anatoa sadaka ya amani na sadaka yake ni ngombe dume au dike, nyama huyo asikuwe na kilema mbele yangu.


Ikiwa anamutolea Yawe sadaka ya kuteketezwa ya ndege, basi, ataleta sadaka yake ya hua au kitoto cha njiwa.


Moyo wangu unaugua kwa ajili ya inchi ya Moabu; wakimbizi wake wanakimbilia Zoari, wanakimbia mpaka Egilati-Selisiya. Wanapanda njia ya kwenda Luhiti wakilia, katika njia kwenda Horonaimu wanatoa kilio cha maangamizi.


Yeye anasema: “Munikusanyie waaminifu wangu, waliofanya agano nami kwa njia ya sadaka!”


Kama hawezi kutoa mwana-kondoo, basi, ataleta hua wawili au vitoto viwili vya njiwa; mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na mwingine kwa ajili ya sadaka ya zambi. Kuhani atamufanyia mama huyo ibada ya upatanisho, naye atakuwa safi.


ngombe dume mumoja na kondoo dume mumoja kwa ajili ya sadaka ya amani, wamutolee Yawe sadaka pamoja na sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa maana leo Yawe atawatokea.


Kama sadaka yake ya kuteketezwa ataitwaa katika kundi la kondoo au mbuzi, basi atachagua dume asiyekuwa na kilema.


Kama sadaka mutu anayotoa ni ya kuteketezwa kwa moto, atamuchagua nyama dume asiyekuwa na kilema kutoka kundi lake, atamutolea mbele ya mulango wa hema la mukutano kusudi apate kukubaliwa na Yawe;


Halafu Abrahamu akainua macho, akaona kondoo dume, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi, akakwenda, akamutwaa yule kondoo, akamutoa sadaka ya kuteketezwa kwa moto pahali pa mwana wake.


Lakini Abramu akamwambia: “Ee Yawe, nitajua namna gani kwamba nitarizi inchi hii?”


Abramu akamuletea hao wote, akakata kila nyama vipande viwili, akavipanga katika mistari miwili, vikielekeana. Lakini ndege hakuwakata vipande viwili.


Siku za kutakaswa kwake zitakapotimia, ikuwe amepata mutoto mwanaume au mwanamuke, atamuletea kuhani kwenye mulango wa hema la mukutano mwana-kondoo wa mwaka mumoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa na kitoto cha njiwa au hua, kwa ajili ya sadaka ya zambi.


maua yamechanua kila pahali. Wakati wa kuimba umefika; sauti za njiwa zinasikilika katika mashamba yetu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite