Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 15:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Yawe akamupeleka Abramu inje na kumwambia: “Angalia mbinguni! Uhesabu nyota, kama kweli utaweza kuzihesabu! Hivi ndivyo wazao wako watakavyokuwa wengi!”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 15:5
22 Referans Kwoze  

Kwa sababu hiyo, kwa njia ya mutu mumoja aliyekuwa akingojea kufa, kukazaliwa wazao wengi sana kama nyota na kama muchanga unaokuwa kandokando ya bahari.


Abrahamu aliamini na kutumainia mambo ambayo yasingewezekana kutumainia na hivi akakuwa babu ya mataifa mengi, kufuatana na maneno haya Mungu aliyomwambia: “Hivi ndivyo wazao wako watakavyokuwa wengi.”


Yawe, Mungu wenu, amewafanya mukuwe wengi; leo mumekuwa wengi kama vile nyota za mbinguni.


Uwakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe, ukisema: Nitawazidisha wazao wenu kama nyota za mbinguni na inchi yote hii niliyowaahidia nitawapa vizazi vyenu wairizi milele.


hakika nitakubariki, na wazao wako nitawazidisha kama nyota mbinguni na kama muchanga pembeni ya bahari. Wazao wako watarizi miji ya waadui zao.


Babu zenu walipokwenda Misri, walikuwa watu makumi saba tu, lakini sasa Yawe, Mungu wenu, amewafanya kuwa wengi kama nyota mbinguni.


Kama vile nyota katika anga na muchanga katika bahari visivyoweza kuhesabiwa, ndivyo nitakavyoongeza hesabu ya wazao wa mutumishi wangu Daudi na hesabu ya makuhani wa ukoo wa Lawi.


Anakadirisha hesabu ya nyota, na kupanga kila moja jina.


Mufalme Daudi hakuwahesabu wale waliokuwa chini ya umri wa miaka makumi mbili kwa maana Yawe aliahidi kuwaongeza Waisraeli kuwa wengi kama nyota za mbinguni.


Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Wazao wako watakuwa wengi kama mavumbi ya dunia, na urizi wao utaenea kila pahali: upande wa magaribi, mashariki, kaskazini na kusini. Kwa njia yako na ya wazao wako, jamaa zote katika dunia zitabarikiwa.


Nitawazidisha wazao wako wakuwe kama nyota za mbinguni na kuwapa inchi hizi zote. Kutokana na wazao wako, mataifa yote katika dunia yatabarikiwa,


Zaidi ya hayo, malaika wa Yawe akamwambia Hagari: “Nitawazidisha wazao wako hata wasiweze kuhesabika kwa wingi wao.”


Wazao wako nitawafanya wakuwe wengi wasihesabike, kama vile mavumbi ya inchi. Kama vile vumbi isivyoweza kuhesabika, ndivyo wazao wako hawataweza kuhesabika!


Nami nitafanya agano nawe na kuwazidisha wazao wako.”


Mimi Mungu nilimwondoa babu yenu Abrahamu kutoka kule ngambo ya muto Furati na kumuleta hapa Kanana, ambako nilimupatia wazao wengi. Nilimupa Isaka,


Na hapa umeniweka kati ya watu wako ambao umewachagua; nao ni wengi hata hawawezi kuhesabika kwa sababu ya wingi wao.


Ukafanya wazao wao kuwa wengi kama nyota za mbinguni; ukawaleta katika inchi uliyowaahidi babu zao.


Basi uangalie mbingu! Angalia mawingu yanayokuwa juu kuliko wewe!


Mukumbuke Abrahamu babu yenu, na Sara aliyewazaa ninyi. Abrahamu alikuwa hana mutoto wakati nilipomwita, lakini nilimubariki na kumufanya kuwa na wengi.


Wewe uliniahidi kunitendea mema na kuwafanya wazao wangu wakuwe wengi kama muchanga wa bahari ambao hauhesabiki kwa wingi wake.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite