Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 15:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Yawe akamwambia Abramu: “Ujue hakika kwamba wazao wako watakaa kama wageni katika inchi isiyokuwa yao, watakuwa watumwa na watateswa kwa muda wa miaka mia ine.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 15:13
26 Referans Kwoze  

Basi, Wamisri wakachagua wakubwa wawasimamie Waisraeli na kuwatesa kwa kazi ngumu. Waisraeli wakafanya kazi ya kumujengea mufalme wa Misri miji ya kuwekea akiba, Pitomu na Ramesesi.


“Siku za kutimiza ahadi Mungu aliyotoa kwa Abrahamu zilipokaribia, hesabu ya watu wa taifa letu kule Misri ikaongezeka hata ikazidika sana.


Mambo ninayotaka kusema ni haya: Mungu amekwisha kufanya agano kwa njia ya haki. Nayo Sheria iliyotokea miaka mia ine makumi tatu nyuma yake haiwezi kulivunja au kugeuza ile ahadi ya Mungu.


Huyo mugeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama vile mwenyeji nawe utamupenda kama vile unavyojipenda mwenyewe, kwa sababu nawe ulikuwa mugeni katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Nitakupa wewe na wazao wako inchi hii ambamo unaishi kama mugeni. Ni kusema inchi yote ya Kanana ikuwe mali yenu milele; nami nitakuwa Mungu wao.”


Basi, muwapende wageni kwa sababu nanyi vilevile mulikuwa wageni katika inchi ya Misri.


Usimutese mugeni. Ninyi munajua hali ya kuwa mugeni, maana mulikuwa wageni katika inchi ya Misri.


Musimutese mujane au yatima.


Wazao wako watarudi hapa katika kizazi cha ine, kwa sababu uovu wa Waamori haujakamilika bado.”


Kisha wakamwambia mufalme: “Sisi watumishi wako tumekuja kukaa kama wageni katika inchi kwa sababu njaa ni kali kule Kanana na hakuna tena malisho kwa nyama wetu. Hivyo, bwana, tunakuomba, sisi watumishi wako, uturuhusu kukaa katika eneo la Goseni.”


Basi, Wamisri wakawatumikisha Waisraeli kwa kinguvu.


Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, Isaka, na Yakobo.


na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Sasa, nitakutuma kwa mufalme wa Misri kusudi uwatoe watu wangu, watu wale wa Israeli, kutoka katika inchi ya Misri.”


Ninaahidi kwamba nitawatoa katika mateso yenu kule Misri na kuwapeleka katika inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. Nitawapeleka katika inchi inayotiririka maziwa na asali.’


Usisahau kwamba wewe ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri, nami Yawe, Mungu wako, nikakutoa huko kwa mukono wenye nguvu na mukono ulionyooshwa. Ndiyo maana mimi Yawe, Mungu wako, nimekuamuru kushika siku ya Sabato.


Alikumbuka ahadi yake takatifu aliyomupa Abrahamu mutumishi wake.


Wakayafanya maisha yao kuwa magumu kwa kazi ngumu ya kutengeneza chokaa na kufyatua matofali, na kazi zote za shamba. Katika kazi zile zote, Waisraeli walitumikishwa kwa kinguvu.


Jinsi babu zetu walivyokwenda Misri, ambako tuliishi kwa muda murefu na jinsi Wamisri walivyowatesa babu zetu, wakatutesa na sisi vilevile.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite