Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 14:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Basi, wale walioshinda, wakanyanganya mali yote ya Sodoma na Gomora, hata na mazao yao, wakajiendea.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 14:11
8 Referans Kwoze  

Mufalme wa Sodoma akamwambia Abramu: “Unipe wale watu, lakini ujitwalie mali yote wewe mwenyewe.”


Basi, Abramu akakomboa mali yote iliyonyanganywa na waadui, na kumukomboa mwipwa wake Loti, mali yake, pamoja na wanawake na watu wengine.


Watakula ngombe wenu na mazao yenu, mpaka muangamie. Hawatawaachia ngano, divai, mafuta, ngombe au kondoo mpaka wawaangamize.


Yawe atashambulia magoti yenu na miguu yenu kwa majipu makali ambayo hamutaweza kuponywa; yatawaenea tangu juu ya kichwa mpaka kwenye vikanyagio vya miguu.


Ngombe wenu watachinjwa mbele ya macho yenu lakini hamutaonja hata kipande cha nyama yao. Punda wenu watatwaliwa kwa nguvu mbele ya macho yenu wala hamutarudishiwa. Kondoo wenu watapewa waadui zenu, na hakuna mutu atakayeweza kuwasaidia.


Alitwaa Sarai muke wake, na Loti mwana wa ndugu yake, pamoja na mali yao yote na watu wote waliokuwa wamejipatia kule Harani, wakaondoka kuelekea inchi ya Kanana. Walipoingia katika inchi ya Kanana,


Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya kabulimbo; kwa hiyo wafalme wa Sodoma na Gomora walipokuwa wakikimbia vita, wakatumbukia mule, lakini wengine wakatorokea kwenye mulima.


Wakamukamata hata Loti mwana wa ndugu ya Abramu aliyekuwa anakaa Sodoma, pamoja na mali yake, wakajiendea.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite