Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 12:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Abramu akapita katikati ya inchi mpaka Sekemu, pahali patakatifu, penye muti wa mwelo wa More. Wakati ule, Wakanana walikuwa ndio wenyeji wa inchi hiyo.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 12:6
20 Referans Kwoze  

Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.


(Milima hii iko ngambo ya muto Yordani, upande wa magaribi wa barabara kuelekea upande jua linakotokea, katika inchi ya Wakanana wanaoishi Araba kuelekea Gilgali.)


Basi, wakamupa Yakobo sanamu zote za miungu ya kigeni walizokuwa nazo pamoja na pete walizokuwa wamevaa kwa masikio. Na Yakobo akavizika chini ya muti wa mwalo uliokuwa karibu na Sekemu.


Yerubali, ni kusema Gideoni na watu wote waliokuwa pamoja naye wakaamuka mapema, wakapiga kambi yao katika bonde karibu na chemichemi ya Harodi. Kambi ya Wamidiani ilikuwa upande wao wa kaskazini katika bonde karibu na mulima More.


Basi, kukatokea ugomvi kati ya wachungaji wa Abramu na wachungaji wa Loti. Wakati ule, Wakanana na Waperizi ndio waliokuwa wenyeji wa inchi hiyo.


Maiti zao zikapelekwa katika jimbo la Sekemu na kuzikwa katika kaburi lile Abrahamu alilonunua kwa feza kutoka kwa wazao wa Hemora.


Akafika karibu na muji mumoja wa Samaria unaoitwa Sikari, uliokuwa karibu na shamba lile Yakobo alilomupa mwana wake Yosefu.


Basi, Rehoboamu akaenda Sekemu ambako Waisraeli wote walikuwa wamekusanyika kwa kumuweka kuwa mufalme.


Abimeleki mwana wa Gideoni, akawaendea wandugu na wana wote wa kabila za mama yake kule Sekemu, akawaambia:


Mifupa ya Yosefu ambayo Waisraeli walikuwa wameileta kutoka Misri waliizika kule Sekemu katika eneo ambalo Yakobo alikuwa amelinunua kutoka kwa wana wa Hamori, baba ya Sekemu, kwa bei ya vikoroti mia moja vya feza. Eneo lile nalo likakuwa mali yao wazao wa Yosefu.


Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.


Basi, Sekemu mwana wa Hamori Muhivi, aliyekuwa mukubwa wa inchi hiyo, alipomwona Dina, akamushika, akalala naye kwa nguvu.


Kutoka Padani-Aramu, Yakobo akafika salama kwa muji wa Sekemu, katika inchi ya Kanana, akapiga kambi yake karibu na muji ule.


Kanana alikuwa babu ya Sidona, muzaliwa wake wa kwanza, na Heti,


Nyuma ya mambo hayo, mufalme Yeroboamu akaujenga upya muji wa Sekemu kwenye mulima wa Efuraimu. Akakaa kule. Kisha akaenda kujenga muji wa Penueli.


Uwaarifu kwa vitambulisho wale wanaokuheshimu, wapate kuuepuka mushale.


Basi, Yakobo akamwambia Simeoni na Lawi: “Ninyi mumeniletea taabu kwa kunifanya nichukiwe na wakaaji wa inchi hii ya Wakanana na Waperizi. Mimi sina watu wengi, na kama wakikusanyika kwa kunishambulia wataniangamiza mimi pamoja na jamaa yangu.”


Kama vile wanyanganyi wanavyomuvizia mutu katika njia, ndivyo makuhani walivyojikusanya na kuvizia. Wanaua watu katika njia yenye kuelekea Sekemu, na kutenda uovu mukubwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite