Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 12:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kwa hiyo, Abramu akaondoka kama vile Yawe alivyomwamuru, na Loti akakwenda pamoja naye. Abramu alikuwa na umri wa miaka makumi saba na mitano alipotoka Harani.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 12:4
10 Referans Kwoze  

Kwa njia ya imani, Abrahamu alitii wakati Mungu alipomwita na kwenda katika inchi ile Mungu aliyoahidi kumupatia kuwa urizi wake. Akaacha inchi yake pasipo kujua pahali anapokwenda.


Tera akatwaa Abramu mwana wake, Loti mujukuu wake aliyekuwa mwana wa Harani, na Sarai muke wa Abramu, wakaondoka wote pamoja toka Uri, muji wa Wakaldea, na kwenda katika inchi ya Kanana. Lakini walipofika Harani, wakakaa pale.


Hawa ndio wazao wa Tera, baba ya Abramu, Nahori na Harani. Harani alikuwa baba ya Loti.


Basi Abrahamu akatoka katika inchi ya Wababeli akaenda kukaa Harani. Kisha kufa kwa baba yake, Mungu akamuhamisha tena, akakuja kukaa katika inchi hii munayoishi ndani yake sasa.


Hivi kisha kungojea kwa uvumilivu, Abrahamu akapokea yale Mungu aliyomwahidi.


Kisha, Sarai akamupa Abramu Hagari, mujakazi wake Mumisri, akuwe muke wake. Haya yalitokea nyuma ya Abramu kukaa katika inchi ya Kanana kwa muda wa miaka kumi.


Abramu alikuwa na umri wa miaka makumi nane na sita wakati Hagari alipozaa Isimaeli.


Abrahamu aliishi miaka mia moja makumi saba na mitano.


Yakobo aliondoka Beri-Seba, akaelekea Harani.


Na Loti, ambaye alikwenda pamoja na Abramu, alikuwa na kondoo, na makundi mengi ya nyama na hema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite