Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 12:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 12:2
38 Referans Kwoze  

Tangu wakati ule nimekuwa pamoja nawe kokote ulikokwenda na nimewaangamiza waadui zako wote mbele yako. Nitakufanya kuwa mwenye utukufu kama wakubwa wengine katika dunia.


Ilitendeka hivi kusudi kwa njia ya Yesu Kristo, baraka Mungu aliyoahidi kwa Abrahamu itolewe vilevile kwa watu wa mataifa mengine na hata sisi kwa njia ya imani, tupate kupokea yule Roho aliyeahidiwa na Mungu.


Yeye atakuwa baba wa taifa kubwa na kwa njia yake mataifa yote ya ulimwengu yatabarikiwa!


Tena Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Nguvu. Ujaliwe wazao wengi na kuongezeka. Taifa na kundi la mataifa watatokea kwako na wafalme watatokea katika uzao wako.


Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu, Mungu wa baba yako. Usiogope kwenda Misri. Utakapokuwa kule, nitakufanya kuwa taifa kubwa.


Nitawazidisha wazao wako wakuwe kama nyota za mbinguni na kuwapa inchi hizi zote. Kutokana na wazao wako, mataifa yote katika dunia yatabarikiwa,


Yawe amemubariki sana bwana wangu, naye amekuwa mutu mukubwa. Amemupa makundi ya kondoo na nyama wengi, feza na zahabu, watumishi wanaume na wanawake, ngamia na punda!


Basi mutambue kwamba wazao wa kweli wa Abrahamu ni wale wanaokuwa wenye imani.


Lakini wazao wa Israeli wakaongezeka sana, wakakuwa wengi na wenye nguvu sana, wakaenea kila pahali katika inchi ya Misri.


Wazao wako nitawafanya wakuwe wengi wasihesabike, kama vile mavumbi ya inchi. Kama vile vumbi isivyoweza kuhesabika, ndivyo wazao wako hawataweza kuhesabika!


Yawe akamupeleka Abramu inje na kumwambia: “Angalia mbinguni! Uhesabu nyota, kama kweli utaweza kuzihesabu! Hivi ndivyo wazao wako watakavyokuwa wengi!”


utasema maneno haya mbele ya Yawe, Mungu wako: ‘Baba yangu alikuwa Musuria aliyetangatanga huko na huko, kisha akashuka kwenda Misri akaishi huko kama mugeni. Yeye na jamaa yake walikuwa watu wachache tu walipokuwa huko, lakini wakakuwa taifa kubwa lenye nguvu na watu wengi.


Sasa, usijaribu kunizuia. Uniache niwaangamize kwa kasirani kali. Kisha kutokana nawe nitaunda taifa kubwa.


Wazao wako watakuwa wengi kama mavumbi ya dunia, na urizi wao utaenea kila pahali: upande wa magaribi, mashariki, kaskazini na kusini. Kwa njia yako na ya wazao wako, jamaa zote katika dunia zitabarikiwa.


Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”


Mungu alipoangamiza miji katika bonde ambamo Loti alikuwa anakaa, alimukumbuka Abrahamu kwa kumutosha Loti katika miji hiyo, kusudi Loti asiangamizwe pamoja nayo.


Nyuma ya pale alitahiriwa, na kutahiriwa kwake kulikuwa kitambulisho cha kuhakikisha ile haki Mungu aliyomuhesabia kwa njia ya imani yake. Hivi Abrahamu akakuwa baba wa watu wote wanaoamini, ijapokuwa hawatahiriwi, kusudi wao vilevile wahesabiwe haki.


Nitawapiga kwa ugonjwa mukali na kuwatupilia mbali; lakini, kutokana nawe, nitaunda taifa lingine kubwa, lenye nguvu kuliko wao.


Zaidi ya hayo, watumishi wa mufalme walikuja kumupa pole bwana wetu mufalme Daudi wakisema: ‘Mungu wako alifanye jina la Solomono kuwa lenye sifa kuliko lako; tena akitukuze kiti chake cha kifalme kuliko kiti chako.’ Halafu mufalme akainama juu ya kitanda


Utatuonyesha uaminifu na wema wako sisi wazao wa Abrahamu na wa Yakobo, kama ulivyowaahidi babu zetu tangu zamani.


Nimemuchagua yeye na wazao wake. Yeye atawafundisha wazao wake kushika njia yangu kwa kutenda kwa haki na kwa kufuata sheria yangu, nami nitawatimizia ahadi zangu.”


Sasa Abrahamu alikuwa muzee wa miaka mingi, naye Yawe alikuwa amemubariki katika kila hali.


Nyuma ya kifo cha Abrahamu, Mungu alimubariki mwana wake Isaka. Naye Isaka akaishi karibu na kisima cha Beri-Lahai-Roi.


Ukae katika inchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe na kukubariki. Nitatimiza ahadi niliyomupa baba yako Abrahamu, maana nitakupa wewe na wazao wako inchi hizi zote.


Mungu akamwambia Balamu: Usiende pamoja na watu hawa, wala usiwalaani watu hao maana wamebarikiwa.


Nimepewa amri ya kubariki, naye amebariki wala siwezi kuigeuza.


Aliwabariki watu wake, wakaongezeka; na hesabu ya wanyama wao akaizidisha.


Nitawafanya waishi kandokando ya mulima wangu mutakatifu na kuwabariki. Nitawaletea mvua kwa wakati wake, nazo zitakuwa mvua za baraka.


Enyi watu wa Yuda na watu wa Israeli! Wakati uliopita ninyi mulionekana kuwa watu waliolaaniwa kati ya watu wa mataifa. Lakini sasa mimi nitawaokoa, nanyi mutakuwa watu waliobarikiwa. Basi, musiogope tena, lakini mujipe moyo!


“Na juu ya Isimaeli, nimesikia ombi lako. Nitamubariki, nitamujalia watoto wengi na kuwazidisha sana. Isimaeli atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, nami nitamufanya kuwa baba wa taifa kubwa.


Uovu wako utamuzuru mwanadamu kama wewe, haki yako itamufalia mwanadamu mwenzako.


Mukumbuke Abrahamu babu yenu, na Sara aliyewazaa ninyi. Abrahamu alikuwa hana mutoto wakati nilipomwita, lakini nilimubariki na kumufanya kuwa na wengi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite