Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 12:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Alipokaribia Misri, Abramu akamwambia Sarai muke wake: “Ninajua kwamba wewe ni mwanamuke muzuri na wa kuvutia.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 12:11
14 Referans Kwoze  

Watu wa kule walipomwuliza juu ya muke wake, akajibu: “Huyu ni dada yangu.” Aliogopa kusema kwamba ni muke wake kwa kuogopa kwamba wakaaji wa inchi wangemwua kwa sababu ya Rebeka, maana Rebeka alikuwa muzuri sana.


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Lea alikuwa na macho zaifu, lakini Rakeli alikuwa muzuri na wa kupendeza.


Basi, Abramu alipofika Misri, wenyeji wa kule wakaona kwamba Sarai ni mwanamuke muzuri sana.


Mupenzi wangu ni kama maua ya hina yanayochanua kwenye mashamba ya mizabibu kule Engedi.


Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo.


Akiwa kule, Abrahamu alisema kwamba muke wake Sara ni dada yake. Kwa hiyo, mufalme Abimeleki wa Gerari akamutwaa Sara.


Binti yule alikuwa na sura ya kuvutia sana na alikuwa angali bikira. Basi, akateremuka kwenye kisima, akaujaza mutungi wake maji na kupanda.


wana wa Mungu wakaona kwamba wale wabinti za watu ni wazuri, wakawatwaa wale waliowapendeza kuwa wake zao.


Wakati Mungu aliponifanya niache nyumba ya baba yangu na kwenda kutangatanga, nilimwambia muke wangu: ‘Popote tutakapokwenda, tafazali useme kwamba mimi ni kaka yako!’ ”


Mutu yule aliitwa Nabali na muke wake aliitwa Abigaili. Abigaili alikuwa mwanamuke mwenye akili na sura nzuri. Lakini Nabali alikuwa mutu wa chuki na mutenda maovu; tena alikuwa wa ukoo wa Kalebu.


Binti yule, alikuwa muzuri sana. Basi, akaanza kumutumikia na kumutunza mufalme, lakini mufalme hakumujua kimwili.


Kuogopa watu ni kujitega mwenyewe, lakini anayemutumainia Yawe yuko salama.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite