Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 10:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Wana wa Semu walikuwa Elamu, Asuri, Aripakisadi, Ludi na Aramu.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 10:22
19 Referans Kwoze  

Nitaweka kati yao kitambulisho cha uwezo wangu. Watakaookolewa kati yao nitawapeleka kwa watu wa mataifa kule Tarsisi, Puti, Ludi, inchi zenye wafundi wa kupiga upinde; watakwenda vilevile Tubali na Ugriki na katika visanga vya mbali ambapo watu hawajapata kusikia habari zangu wala kuuona utukufu wangu. Wale wajumbe wangu watautangaza utukufu wangu katika mataifa hayo.


Kati yetu kuna watu wenye kutoka katika inchi hizi: Parti, Medi, Elamu, Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto, Jimbo la Azia,


wafalme wote wa Simuri, Elamu na Medi;


Majeshi ya Elamu, pinde na mishale katika mikono, walikuja wamepanda farasi na magari ya vita; nalo jeshi la Kiri lilitayarisha ngao zake.


Nimeonyeshwa maono ya kutisha: wadanganyifu wanadanganya na waangamizaji wanaangamiza. Mupande kwa kupigana vita, enyi Waelamu! Mushambulie, enyi Wamedi! Mungu atakomesha mateso yote yaliyoletwa na Babeli.


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Yule naye alipokuwa hajamaliza kusema, mwingine akafika, akasema: “Wakaldea walijipanga makundi matatu, wakashambulia ngamia, wakawatwaa, na wakaua watumishi wako kwa upanga! Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


Basi, Puli mufalme wa Asuria akashambulia inchi ya Israeli, naye Menahemu akamupa kilo elfu makumi tatu na ine za feza kusudi amusaidie kuimarisha mamlaka yake juu ya inchi ya Israeli.


Balamu akamutolea Balaki mashairi yake, akasema: Balaki amenileta hapa kutoka Aramu, hakika, mufalme wa Moabu amenileta kutoka milima ya mashariki: Kuja uwalaani watu wa Yakobo kwa ajili yangu, hakika, kuja uwakaripie Waisraeli!


Tena akasema: “Semu abarikiwe na Yawe, Mungu wangu! Kanana akuwe mutumwa wake.


Semu, mukubwa wa Yafeti, alikuwa baba ya Waebrania wote.


Hawa ndio wazao wa Semu. Miaka miwili nyuma ya yale mafuriko ya maji, Semu akiwa na umri wa miaka mia moja, alizaa Aripakisadi.


Lakini mutateketezwa, enyi Wakeni. Mutapelekwa mateka na Asuria mpaka wakati gani?


Elamu nayo iko huko. Makaburi ya waaskari wake yanaizunguka. Wote waliuawa katika vita. Wakashuka kwenye inchi ya wafu, bila kujua Mungu. Walipokuwa wangali wanaishi, walieneza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima. Lakini sasa wanapata haya yao pamoja na wale wanaoshuka katika shimo kwa wafu.


Katika maono haya, nilijikuta niko Susani, muji mukubwa wa jimbo la Elamu. Nilikuwa nimesimama kando ya muto Ulayi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite