Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 10:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Wana wa Yafeti walikuwa Gomeri, Magogi, Madayi, Yavani, Tubali, Meseki na Tirasi.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 10:2
16 Referans Kwoze  

Wewe mwanadamu! Umugeukie Gogi mufalme wa inchi ya Magogi ambaye ni mutawala mukubwa wa Meseki na Tubali.


Vilevile makundi ya waaskari kutoka Gomeri, Beti Torgama, upande wa kaskazini kabisa, na makundi yao yote pamoja na makundi kutoka katika mataifa mengine, yako pamoja nawe.


naye atakwenda kuwadanganya watu wa mataifa wanaokuwa katika pande zote za dunia, ndio wanaoitwa Gogi na Magogi. Shetani atawakusanya kwa kupigana vita, nao watakuwa wengi kama vile muchanga wa bahari.


Nitaweka kati yao kitambulisho cha uwezo wangu. Watakaookolewa kati yao nitawapeleka kwa watu wa mataifa kule Tarsisi, Puti, Ludi, inchi zenye wafundi wa kupiga upinde; watakwenda vilevile Tubali na Ugriki na katika visanga vya mbali ambapo watu hawajapata kusikia habari zangu wala kuuona utukufu wangu. Wale wajumbe wangu watautangaza utukufu wangu katika mataifa hayo.


Bwana wetu Yawe akaniambia: Wewe mwanadamu! Toa unabii juu ya Gogi. Useme: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana nawe Gogi mutawala mukubwa wa mataifa ya Meseki na Tubali.


kutoka kwenye makao yako, huko mbali kabisa upande wa kaskazini, ukuje pamoja na watu wengi wakiwa wote wamepanda farasi: jeshi kubwa na lenye nguvu.


Wedani na Yavani walisafirisha vitu vyako toka muji wa Uzali; hata chuma kilichofuliwa, mudalasini na muchaichai kwa kununua vitu kwako.


Kitani kilichopindwa vizuri kutoka Misri kilikuwa kwa kupamba tanga lako na kwa ajili ya bendera yako. Chandarua chako kilitengenezwa na nguo ya rangi ya samawi na nyekundu-nyeusi kutoka visanga vya Elisa.


Semu, mukubwa wa Yafeti, alikuwa baba ya Waebrania wote.


Mungu amuzidishe Yafeti, aishi katika hema za Semu; Kanana akuwe mutumwa wake.”


Nyuma ya mafuriko ya maji, Semu, Hamu na Yafeti, wana wa Noa, walipata watoto wanaume na wanawake. Hawa ndio wazao wao:


Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.


Ole wangu maana ninaishi kama mugeni huko Meseki; ninaishi kama mugeni katika mahema ya Kedari.


Mesaki na Tubali ziko huko. Makaburi ya watu wake wote yanazizunguka. Wote waliuawa katika vita, bila kujua Mungu. Walipokuwa wangali wanaishi, walieneza vitisho vyao katika inchi ya wanaokuwa wazima.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite