Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 1:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Kisha Mungu akasema: “Tumufanye mutu kwa mufano wetu, anayefanana nasi, atawale samaki wa bahari, ndege wa anga, nyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vinavyotambaa.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 1:26
34 Referans Kwoze  

na kuvaa utu mupya. Utu ule unaendelea kufanywa upya kila mara kufuatana na mufano wa Mungu anayekuwa muumba wake, kusudi mupate kumujua hakika.


Mukuwe na hali mupya, inayoumbwa kwa mufano wa Mungu na inayoonekana katika maisha ya haki na utakatifu wa kweli.


Kisha Yawe Mungu akasema: “Sasa, mwanadamu amekuwa kama mumoja wetu, anajua mazuri na mabaya. Inafaa kumuzuia kula lile tunda la muti wa uzima, maana akilikula ataishi milele.”


Hiki ndicho kitabu cha uzao wa Adamu. Wakati Mungu alipowaumba wanadamu, aliwaumba kwa mufano wake.


Mujue kwamba Yawe ndiye Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, sisi ni mali yake; sisi ni watu wake na kondoo wake anaowachunga.


Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.


Usitukasirikie sana, ee Yawe, usiukumbuke uovu wetu siku zote! Ukumbuke kwamba sisi wote ni watu wako!


Kristo ni mufano kamili wa Mungu asiyeonekana. Yeye ni muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.


Kwa njia ya ulimi tunamusifu Bwana anayekuwa Baba yetu, na kwa njia ile ile tunalaani watu walioumbwa kwa mufano wa Mungu.


Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.


Mwanaume hapaswi kufunika kichwa, kwa sababu yeye ni mufano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamuke ni utukufu wa mwanaume.


Anayemwanga damu ya mwanadamu, damu yake itamwangwa na mwanadamu; maana mwanadamu aliumbwa kwa mufano wa Mungu.


Nimetambua jambo hili moja: kwamba Mungu aliwaumba wanadamu wenye usawa, lakini wao wenyewe wamejitafutia matatizo.


Kutokana na mutu mumoja, yeye aliumba watu wa mataifa yote kusudi waishi katika dunia yote. Aliwapangia nyakati na kukata mipaka ya inchi wanayopaswa kukaa ndani yake.


Yesu akamujibu: “Anayenipenda, atashika maneno yangu. Baba yangu atamupenda, naye Baba pamoja nami tutaingia ndani yake na kukaa ndani yake.


Maana kuna washuhuda watatu:


Kila namna ya nyama, ndege, nyoka na samaki wanaweza kufugwa na mutu, na wamekwisha kufugwa naye.


Kisha nikamusikia Yawe akisema: Nimutume nani? Ni nani atakayekuwa mujumbe wetu? Nami nikajibu: Niko hapa! Unitume mimi.


Umufurahie Muumba wako, ee Israeli; ninyi wakaaji wa Sayuni, mumushangilie mufalme wenu.


Basi, tushuke chini na kuvuruga luga yao kusudi wasielewane wao kwa wao.”


Sasa nimetoa inchi zote kwa mutumishi wangu Nebukadneza mufalme wa Babeli. Vilevile nimemupa nyama wa pori wamutumikie.


Lakini hakuna anayesema: “Yuko wapi Mungu, Muumba wangu, mwenye kunifanya nichangamuke usiku,


Lakini Yesu akawajibu: “Baba yangu anatumika wakati wote, nami ninatumika vilevile.”


Kwa maana unatuelezea mambo ya kigeni. Basi tunataka kujua maana yake.”


Nawe utapatana na mawe ya shamba, na nyama wakali watakuwa na amani nawe.


Basi, Yawe akaumba kutoka udongo kila nyama wa pori na kila ndege wa anga, halafu akamuletea yule mwanaume aone atawapa majina gani. Na majina aliyowapa viumbe hao, yakakuwa ndiyo majina yao.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.


Utamutegemea kwa sababu ana nguvu nyingi na kumwacha akufanyie kazi zako nzito?


Tutakufanyizia mikufu ya zahabu, iliyopambwa vizuri kwa feza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite