24 Mungu akasema: “Inchi itoe aina zote za viumbe vyenye uzima: nyama wa kufugwa, viumbe vinavyotambaa na nyama wa pori wa kila aina.” Ikakuwa hivyo.
Uangalie yule nyama mukubwa kiboko. Nilimwumba kama nilivyokuumba wewe. Yeye anakula majani kama ngombe,
“Utaingiza kila aina ya ndege wa anga, kila aina ya nyama, kila aina ya kiumbe kinachotambaa, wawili wa kila aina, kwa kuwalinda wazima.
Wakatoka, kufuatana na jamii zao, nyama wote wa pori, viumbe vyote vinavyotambaa, ndege wote na nyama wote wenye uzima katika dunia.
Mumusifu, enyi nyama wa pori na wa kufugwa, viumbe vinavyotambaa na ndege wote!
Nani aliyemwacha huru punda wa pori? Nani aliyewaacha waende kwa kuwafungua?
Waliingia wao wenyewe pamoja na aina zote za nyama wa pori, aina zote za nyama wanaofugwa, aina zote za nyama wanaotambaa na ndege wa kila aina.
Hapo mwanadamu naye anaenda kwenye kazi zake; naye anatumika mpaka magaribi.
Milima mirefu ni makao ya mbuzi wa pori; makimbilio ya sungura wa pori ni chini ya mawe.
Yobu, ni wewe ndiwe uliyewapa farasi nguvu, ukawavalisha kwenye shingo manyoya marefu?
Mbogo atakubali kukutumikia? Atakubali kulala katika zizi lako?
Unajua mbuzi wa milima anazaa wakati gani, au umekwisha kuona kulungu akizaa?
Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya tano.
Basi, Yawe akaumba kutoka udongo kila nyama wa pori na kila ndege wa anga, halafu akamuletea yule mwanaume aone atawapa majina gani. Na majina aliyowapa viumbe hao, yakakuwa ndiyo majina yao.