Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 1:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Mungu akavibariki, akasema: “Muzae, muongezeke, mujaze maji ya bahari, nao ndege waongezeke katika inchi.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 1:22
16 Referans Kwoze  

Ondoa vilevile viumbe vyote vyenye uzima vya kila aina vilivyokuwa pamoja nawe, ndege na nyama na kila kiumbe kinachotambaa, vipate kuzaa kwa wingi katika dunia, viongezeke na kuenea kila pahali katika dunia.”


Aliwabariki watu wake, wakaongezeka; na hesabu ya wanyama wao akaizidisha.


Uangalie yule nyama mukubwa kiboko. Nilimwumba kama nilivyokuumba wewe. Yeye anakula majani kama ngombe,


Mungu akawabariki na kuwaambia: “Muzae, muongezeke, na mujaze inchi na kuitawala. Mutawale samaki wa bahari, ndege wa anga, na kila kiumbe chenye uzima kinachotembea katika dunia.”


Katika miaka ya Yobu iliyofuata, Yawe alimubariki zaidi kuliko hata alivyokuwa amemubariki pale mbele. Basi Yobu akakuwa na kondoo elfu kumi na ine, ngamia elfu sita, ngombe elfu mbili na punda dike elfu moja.


Mungu akamubariki Noa na wana wake, akiwaambia: “Muzae, muongezeke, mujaze inchi.


Baraka za Yawe ndizo zinazoleta utajiri. Juhudi za mutu haziongezi kitu.


Muke wako atakuwa kama muzabibu wenye matunda mengi; watoto wako kama vichipukizi vya muzeituni kuzunguka meza yako.


Mumushukuru Yawe kwa wema wake na maajabu yake kwa wanadamu.


Nitawarehemu na kuwajalia mupate watoto wengi na kuongezeka. Nami nitaliimarisha agano langu nanyi.


Tena Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Nguvu. Ujaliwe wazao wengi na kuongezeka. Taifa na kundi la mataifa watatokea kwako na wafalme watatokea katika uzao wako.


Mbele sijakuja ulikuwa na mali chache tu lakini tangu nifike, mali yako imeongezeka kwa wingi sana, na Yawe amekubariki kila fasi nilikokwenda. Lakini sasa, nitatunza wakati gani jamaa yangu mwenyewe?”


Lakini Labani akamwambia: “Basi uniruhusu nami niseme. Nimetambua kwa kuaguza kwamba Yawe amenibariki kwa sababu yako.


Mungu akaumba nyama wakubwa sana wa bahari na aina zote za viumbe vyenye uzima vinavyotembea ndani ya maji. Akaumba aina zote za ndege. Mungu akaona kwamba ni vizuri.


Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya tano.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite