Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 1:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Mungu akafanya miangaza miwili mikubwa: ule mukubwa utawale muchana na ule mudogo utawale usiku. Akafanya nyota vilevile.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 1:16
22 Referans Kwoze  

Mufanye angalisho kusudi wakati mutakapoangalia na kuona nyota, vitu vyote vya mbinguni, musivutwe kuviabudu na kuvitumikia. Vitu hivyo Yawe amewaachia watu wengine waviabudu.


Kutoka maneno ya watoto wadogo, hata wachanga, unaimarisha nguvu mbele ya waadui zako na kuwakomesha waasi na wapinzani wako.


Muinue macho yenu juu mbinguni! Ni nani aliyeziumba nyota hizo? Ni yule anayeziongoza kama jeshi lake, anayeijua hesabu yake yote, anayeziita kila moja kwa jina lake. Kwa sababu yeye ni mwenye nguvu nyingi, hakuna hata moja inayokosekana.


Vyote visifu jina la Yawe, maana yeye aliamuru, na vyote vikakuwa.


Muchana ni wako na usiku ni wako; umeweka mwezi na jua kwenye nafasi zao.


Mumusifu enyi jua na mwezi, mumusifu enyi nyota zote zinazoangaza.


nyota za asubui zilipokuwa zikiimba pamoja, na wana wa Mungu wakapiga vigelegele vya shangwe?


Uzuri wa jua ni mbalimbali na uzuri wa mwezi, nao uzuri wa nyota ni mbalimbali, kwa maana hata nyota zinapishana uzuri vilevile.


Tangia saa sita ya muchana, giza lilikuwa katika inchi yote mpaka saa tisa.


Jua na mwezi vilikaa kimya katika makao yao, vilipoona mwangaza wa mishale yako ikienda mbio, vilipouona mukuki wako ukimetameta.


Mimi ninafanya mwangaza na kuumba giza; ninaleta uheri na kusababisha hasara. Mimi Yawe ninatenda vitu hivi vyote.


Nyota na vikundi vyake katika anga hazitaangaza; jua linapochomoza litakuwa giza, na mwezi hautatoa mwangaza wake.


nalo linatoka kama vile bwana-arusi kutoka chumba chake, linakimbia kwa furaha katika njia yake kama shujaa.


Muji ule hauna lazima ya mwangaza wa jua, wala wa mwezi, kwa sababu utukufu wa Mungu unauangazia na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.


Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.


Sikuangalia jua likiangaza au mwezi ukipita katika uzuri wake


“Mara moja kisha mateso ya siku zile, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka toka mbinguni na vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.


na iangae katika anga na kuangazia dunia.” Ikakuwa hivyo.


Yawe, yule aliyepanga jua liangaze muchana, mwezi na nyota viangaze usiku, na anayevumisha mawimbi ndani ya bahari, yule ambaye jina lake ni Yawe wa majeshi, anasema hivi:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite