Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Inchi ikaotesha mimea inayozaa mbegu za aina yake, na miti inayozaa matunda yenye mbegu za aina yake. Mungu akaona kwamba ni vizuri.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 1:12
11 Referans Kwoze  

Udongo wenyewe unaotesha mimea; kwanza majani, halafu masuke na kisha ngano zinazokomaa ndani ya masuke.


Kwa maana kila muti unajulikana kwa njia ya matunda yake. Watu hawachumi matunda ya tini au mizabibu juu ya miti ya miiba.


Musidanganyike: Mungu hachekelewi. Chochote mutu atakachopanda, ndicho atakachovuna.


Mungu ndiye anayemupatia mupandaji mbegu na mukate wa kukula. Kwa hiyo atawapatia ninyi mbegu yoyote munayohitaji na kuiotesha, kusudi moyo wenu wa kutoa upate kuzaa matunda mengi.


Hivyo, kama vile udongo unavyootesha mimea, na shamba linavyochipukiza mbegu zilizopandwa humo, Yawe atasababisha haki na sifa kuonekana mbele ya mataifa yote.


Udongo unaonyeshewa na mvua mara kwa mara na kutoa mimea inayofaa kwa walimaji, unabarikiwa na Mungu.


Kisha Mungu akasema: “Inchi ioteshe mimea: mimea inayozaa mbegu, na miti inayozaa matunda yenye mbegu za aina yake.” Ikakuwa hivyo.


Ikakuwa magaribi na kisha ikakuwa asubui, ndiyo siku ya tatu.


Unaotesha majani kwa ajili ya mifugo, na mimea kwa matumizi ya mwanadamu kusudi naye apate chakula chake toka udongo:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite