Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kisha Mungu akasema: “Inchi ioteshe mimea: mimea inayozaa mbegu, na miti inayozaa matunda yenye mbegu za aina yake.” Ikakuwa hivyo.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 1:11
20 Referans Kwoze  

Udongo unaonyeshewa na mvua mara kwa mara na kutoa mimea inayofaa kwa walimaji, unabarikiwa na Mungu.


Yeye anafunika anga kwa mawingu, anaitayarishia inchi mvua, na kuchipukiza nyasi kwenye vilima.


Kisha Mungu akasema: “Ninawapa kila mumea katika dunia unaozaa mbegu na kila muti unaozaa matunda yenye mbegu, kwa ajili ya chakula chenu.


Yawe Mungu akaotesha kutoka udongo kila aina ya miti ya kupendeza macho na inayofaa kwa chakula. Katikati ya bustani hiyo kulikuwa muti wa uzima na muti wa kujua mazuri na mabaya.


Udongo wenyewe unaotesha mimea; kwanza majani, halafu masuke na kisha ngano zinazokomaa ndani ya masuke.


Basi ikiwa Mungu anavalisha majani kama hivi, yanayoonekana leo na kesho yanatoweka na kutupwa katika moto, hatawavalisha ninyi vizuri zaidi, ninyi wenye imani ndogo?


Kutoka ndani ya udongo chakula kinapatikana, lakini chini yake kila kitu kinavurugwa kwa moto.


Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito, unaozaa matunda kwa wakati wake, na majani yake hayanyauki hata kidogo. Anafanikiwa katika yote anayofanya.


hakukukuwa mimea juu ya inchi wala miti haikukuwa imeota maana Yawe Mungu hakukuwa ameinyeshea inchi mvua, wala hakukukuwa mutu wa kuilima.


Wandugu zangu, muti unaotoa matunda ya tini unaweza kutoa matunda ya muzeituni? Au muzabibu unaweza kutoa matunda ya tini? Hapana! Hivi vilevile kisima kinachotoa maji ya chumvi hakiwezi kutoa maji matamu.


Shoka limekwisha kuwekwa tayari kwenye mashina ya miti. Kila muti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa katika moto.


Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya maji, unaopenyeza mizizi yake karibu na chemichemi. Hauogopi wakati wa jua kali, majani yake yanabaki mabichi. Hauhangaiki katika mwaka wa ukosefu wa mvua, nao haukosi kuzaa matunda.


Yawe Mungu akamwamuru yule mwanaume: “Unaweza kula matunda ya muti wowote katika bustani.


Mungu anatokeza ndani ya ile punje umbo la mumea anaotaka; yeye anatokeza ndani ya kila mbegu umbo la kipekee.


Inchi ikaotesha mimea inayozaa mbegu za aina yake, na miti inayozaa matunda yenye mbegu za aina yake. Mungu akaona kwamba ni vizuri.


Hivyo, kama vile udongo unavyootesha mimea, na shamba linavyochipukiza mbegu zilizopandwa humo, Yawe atasababisha haki na sifa kuonekana mbele ya mataifa yote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite