10 Mungu akapaita pahali pakavu “Inchi” na kusanyiko la maji akaliita “Bahari”. Mungu akaona kwamba ni vizuri.
Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.
Utukufu wa Yawe unadumu hata milele; Yawe anapendezwa na matendo yake mwenyewe.
Mungu akaona kwamba mwangaza ule ni muzuri. Kisha Mungu akatenganisha mwangaza na giza.
Alikusanya maji ya bahari kama katika chupa, akavifunga vilindi vya bahari ndani ya gala.
Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya; kwa mikono yake aliumba inchi kavu.
aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao. Yeye anashika ahadi yake milele.
Yona akawajibu: Mimi ni Mwebrania; ninamwabudu Yawe, Mungu wa mbingu, muumba wa bahari na inchi kavu.