Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 9:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Maana, wanaoishi wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui kitu chochote. Hawana malipo tena. Hakuna ukumbusho juu yao, wamesahauliwa kabisa.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 9:5
18 Referans Kwoze  

Watu hao wamekufa, wala hawataishi tena; wamekuwa mizimu, wala hawatafufuka. Maana wewe umewaazibu na kuwaangamiza, hakuna atakayeweza kuwakumbuka tena.


Hakuna mutu anayekumbuka mambo ya zamani, wala atakayekumbuka yatakayotukia kisha.


Unigeukie, ee Yawe, uniokoe; uniponyeshe kwa sababu ya wema wako.


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Watoto wake wakiheshimika, yeye hana habari. Wakizarauliwa, yeye haoni kabisa.


Maana hakuna anayemukumbuka mwenye hekima, wala anayemukumbuka mupumbafu, maana katika siku zinazokuja wote watasahaulika. Maana mwenye hekima anakufa sawasawa na mupumbafu!


Yawe akumbuke zambi zao siku zote; lakini wao wenyewe wasahauliwe katika dunia.


Tena, nimeona waovu wakizikwa, watu ambao walizoea kuingia na kutoka pahali patakatifu, na kusifiwa katika muji uleule walimotenda maovu yao. Hayo nayo ni bure.


Maana wewe ndiwe Baba yetu; Abrahamu, babu yetu, hatujali, naye Israeli hatutambui; lakini wewe, ee Yawe, ni Baba yetu. Wewe umeitwa tangu zamani: Mukombozi wetu.


Afazali kwenda kwenye kilio, kuliko kwenda kwenye karamu, kwa sababu inawapasa wenye kuwa wazima kukumbuka kwamba kifo kinawangojea sisi wote.


Kweli! Ninajua utanipeleka tu katika kifo, pahali wote wanaoishi watakapokutana.


Lakini anayeambatana na wanaoishi angali bado na tumaini. Afazali imbwa mwenye kuishi kuliko simba mwenye kufa.


Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.


Sisi wote tutakufa. Sisi ni kama maji yaliyomwangika chini ambayo hayawezi kuzoleka. Lakini Mungu hataki Abusaloma akufe sasa au aendelee kuishi mbali naye.


Maajabu yako yanajulikana humo katika giza, au matendo yako ya haki katika inchi ya waliosahauliwa?


Na kwa mwisho, yule mwanamuke akakufa vilevile.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite