Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 8:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Haya yote nimeyaona katika uchunguzi wangu juu ya yote yanayotendeka hapa chini ya jua, ambako mwanadamu anatawala mwenzake na kumutesa.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 8:9
15 Referans Kwoze  

Faida ya mavuno ya inchi ni kwa watu wote, hata mufalme vilevile anatumainia mavuno yale.


Kwa bahati mbaya, mali hiyo iliharibiwa katika matumizi mabaya. Kwa mwisho, mutu yule hakukuwa na kitu chochote wakati alipokuwa na mwana.


Hata hivyo, nilikusudia kujua na kuchunguza na kutafuta hekima na maana ya mambo yanayokuwa, na vilevile kujua kwamba uovu ni upumbafu na kwamba upumbafu ni wazimu.


Mimi nimeiona kazi ambayo mwanadamu amepewa na Mungu.


Nimeyaona mambo yote yanayofanywa chini ya jua. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo!


“Lakini Sihoni, mufalme wa Hesiboni, hakuturuhusu tupite katika inchi yake. Yawe, Mungu wenu, akamufanya akuwe na kichwa kigumu na mugumu wa moyo, kusudi tumushinde na kutwaa inchi yake ambayo tunairizi mpaka leo.


Maji yakafunika magari pamoja na wapanda-farasi. Jeshi lote la mufalme wa Misri lililokuwa limewafuatilia Waisraeli likakufa katika bahari. Hakukuponyoka Mumisri hata mumoja.


Halafu wakawaua wana wa Zedekia mbele yake, kisha wakamwongoa macho yake. Kwa mwisho wakamufunga kwa minyororo, wakamupeleka Babeli.


Zaidi ya hayo, nimegundua chini ya jua kwamba uovu unatawala kwa pahali pa haki na sheria.


Kisha nikaona mateso yote yanayofanyika chini ya jua. Watu wanaogandamizwa wanalia machozi, lakini hakuna mutu yeyote anayewafariji. Wagandamizaji wao wana nguvu, ndiyo sababu hakuna wa kuwafariji.


Mwenye hekima akimutesa mutu, yeye anafanya kama mupumbafu. Kupokea kituliro kunapotosha akili.


Usishangae ukiona katika inchi wamasikini wanagandamizwa, wananyimwa haki na sheria zao. Kila mwenye cheo anayewatesa wamasikini yupo chini ya mukubwa mwingine, na juu ya hao wote kuna wakubwa zaidi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite