Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 8:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Anayetii amri hatapata hasara, na mwenye hekima atajua kwamba kuna wakati wa hukumu.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 8:5
21 Referans Kwoze  

Lakini chakula kigumu ni kwa ajili ya watu wazima, ndio wale waliozoeza mafikiri yao hata wapate kutambua mema na mabaya.


Lakini Petro na Yoane wakawajibu: “Muamue ninyi wenyewe, ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumutii Mungu?


Halafu Yesu akawaambia: “Basi mumupe Mufalme wa Roma vinavyokuwa vyake, na Mungu vinavyokuwa vyake.”


Kutoka nusu ya kabila la Manase: watu elfu kumi na nane, waliotajwa majina kwa kuja kumuweka Daudi kuwa mufalme.


Petro na mitume wengine wakajibu: “Inatupasa sisi kumutii Mungu kuliko watu!


Efuraimu ameteswa, haki zake zimetwaliwa; maana alikusudia kufuata mambo isiyokuwa na maana.


Moyo wa mwenye hekima unamwongoza kutenda mambo yanayokuwa sawa; lakini mutu mupumbafu anapotoshwa na moyo wake.


Mimi ninasema hivi: tii amri ya mufalme. Kwa sababu ya kiapo chako kitakatifu, usikate tamaa.


Mwenye hekima anaona anakokwenda, lakini mupumbafu anatembea katika giza. Hata hivyo, ninajua vilevile kwamba mwisho wao wote wawili ni mumoja.


Hekima ni mbele ya uso wa mwenye akili, lakini macho ya mupumbafu yanaangalia kwa miisho ya dunia.


Lakini kwa sababu wazalishaji wale walimwogopa Mungu, hawakufanya kama vile walivyoamuriwa na mufalme, lakini waliwaacha watoto wanaume wa Waisraeli waishi.


Kwa sababu hii hatuchoki kuwaombea ninyi, tangu siku tuliposikia habari zenu. Tunamwomba Mungu awawezeshe kujua kabisa mapenzi yake na kuwajaza hekima na akili inayotoka kwa Roho wake.


Nikichunguza amri zako zote, hapo kweli sitapata haya.


Wenye haki hawapatwi na jambo lolote baya, lakini waovu wanapata hasara nyingi.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite