Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 8:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Amri ya mufalme ni shauri la mwisho. Nani anayesubutu kumwuliza: “Unafanya nini?”

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 8:4
18 Referans Kwoze  

Yeye akitwaa kitu kwa rafla, nani anayeweza kumuzuia? Nani anayeweza kumwuliza: “Unafanya nini?”


Halafu sasa wewe mwanadamu ni nani hata ubishane na Mungu? Chombo cha udongo hakiwezi kumwuliza mufinyanzi: “Kwa nini umenitengeneza hivi?”


Kasirani kali ya mufalme ni kama simba anayenguruma; anayemukasirikisha anahatarisha maisha yake.


Kasirani ya mufalme ni kama ngurumo ya simba, lakini upendo wake ni kama umande juu ya majani.


Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?


jogoo anayetembea kwa maringo, beberu, na mufalme mbele ya watu wake.


Hapo, mufalme akamwamuru Benaya mwana wa Yehoyada, naye akatoka, akamupiga na kumwua Simei. Basi, ufalme ukaimarika chini ya Solomono.


Halafu mufalme Solomono akatoa amri kwa Benaya mwana wa Yehoyada; naye akamwendea Adonia, akamwua.


Basi, mufalme akawaita wazalishaji wale, akawauliza: “Kwa nini mumefanya hivyo? Mbona mumewaacha watoto wanaume waishi?”


Lakini neno la mufalme lilikuwa na nguvu zaidi mbele ya Yoabu na majemadari wa kundi la waaskari. Basi, Yoabu na majemadari wa waaskari wakaondoka mbele ya mufalme, wakaenda kuwahesabu Waisraeli.


kama nilivyokuapia mbele ya Yawe, Mungu wa Israeli, nikisema: ‘Mwana wako Solomono atatawala nyuma yangu, na ataikaa juu ya kiti changu cha kifalme pahali pangu’, ndivyo nitakavyofanya leo.”


Basi, Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi, na wakubwa wenzao, wakafanya bidii kwa kutimiza maagizo ya mufalme.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite