Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 8:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 lakini hataelewa kazi ya Mungu inayofanyika chini ya jua. Mutu anaweza kutoa jasho sana lakini hataelewa. Wenye hekima wanaweza kujidai kwamba wanajua, lakini, kwa kweli, hawajui.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 8:17
13 Referans Kwoze  

Mungu amefanya kila kitu kikuwe kizuri kwa wakati wake. Ameweka ndani ya moyo wa mwanadamu mawazo juu ya muda usiokuwa na mwisho, lakini mutu hawezi kuelewa mwanzo na mwisho wa matendo ya Mungu.


Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!


Basi, nilijaribu kufikiri juu ya jambo hili, lakini lilikuwa gumu sana kwangu,


Ninyi hamujui bado? Hamujapata kusikia? Yawe ndiye Mungu wa milele; yeye ndiye Muumba wa kila kitu katika dunia. Yeye haregei hata kidogo wala kuchoka. Maarifa yake hayachunguziki.


yeye anayetenda mambo makubwa yasiyochunguzika, anayetenda maajabu yasiyohesabika.


Kama vile hauwezi kujua jinsi uzima unavyoingia katika mifupa ya mutoto katika tumbo la mama yake, vilevile hauwezi kuelewa matendo ya Mungu, aliyefanya kila kitu.


Heri mutu anayemutumainia Yawe, mutu asiyejiunga na watu wenye majivuno, watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.


Ee Yawe, matendo yako ni mengi sana! Umeyafanya kwa hekima yote! Dunia imejaa viumbe vyako!


Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.


Mufikiri vema juu ya kazi ya Mungu. Ni nani anayeweza kunyoosha kitu Mungu alichokunja?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite