Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 8:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kuna jambo moja la bure nililotambua hapa katika dunia: mara kwa mara watu wema wanatendewa jinsi waovu wanavyostahili kutendewa, nao waovu wanatendewa jinsi watu wema wanavyostahili kutendewa. Ninasema kwamba hayo nayo ni bure.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 8:14
16 Referans Kwoze  

Katika maisha yangu ya bure, niliona kila kitu. Mutu wa haki anakufa ingawa ni wa haki, ambapo mutu mwovu anaendelea kuishi maisha marefu ingawa ni mwovu.


Tunayoona sisi, ni kwamba wenye kiburi ndio wenye furaha siku zote. Watu waovu, ingawa wanastawi, hata wanapomujaribu Mungu, hawapati azabu.


Mwenye hekima anaona anakokwenda, lakini mupumbafu anatembea katika giza. Hata hivyo, ninajua vilevile kwamba mwisho wao wote wawili ni mumoja.


maana niliwaonea wivu wenye kiburi, nilipoona wakosaji wakifanikiwa.


Kwa nini waovu wanaendelea kuishi? Mbona nguvu zao zinaongezeka hata katika uzee?


Ee Yawe, wewe ni mwenye haki, ingawa nitakushitaki. Lakini ningependa nibishane nawe juu ya mambo ya haki: Kwa nini waovu wanafanikiwa katika mambo yao? Mbona wote wanaodanganya wanastawi?


Kuna uovu niliotambua hapa chini ya jua, uovu unaosababishwa na watawala:


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Tena nilitambua kwamba mutu anatoa jasho na kutumia ujuzi wake juu ya wivu tu kwa mwenzake. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Katika mambo haya yote Yobu hakutenda zambi wala hakumushitaki Mungu kuwa na kosa.


Lakini ninyi munajua jambo lile vizuri sana! Mbona, basi munasema maneno yasiyokuwa na maana?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite