Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 8:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Wenye zambi wanatenda maovu mara mia. Hata hivyo, wanaendelea kuishi. Lakini, mimi ninajua kwamba itakuwa heri kwa wanaomwogopa Mungu, kwa sababu ya woga wao.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 8:12
34 Referans Kwoze  

Lakini wapole watarizi inchi, hao wataifurahia amani kamili.


Basi, ni kusema kwamba Bwana anajua namna ya kuwaokoa wenye kumwogopa katika majaribu. Lakini anangojea kuwaazibu watu wabaya kwa Siku ile ya hukumu.


Katika maisha yangu ya bure, niliona kila kitu. Mutu wa haki anakufa ingawa ni wa haki, ambapo mutu mwovu anaendelea kuishi maisha marefu ingawa ni mwovu.


Ninajua kwamba jambo lolote Mungu analotenda linadumu milele. Hakuna kinachoweza kuongezwa wala kupunguzwa. Mungu amefanya mambo yakuwe hivyo kusudi wanadamu wamwogope yeye.


Basi kuna nini? Mungu alitaka kuonyesha kasirani yake na kutambulisha uwezo wake. Lakini aliwavumilia sana wale waliostahili kupatwa na kasirani yake na waliokuwa wametayarishwa kwa kuangamizwa.


Yeye anawasikilia wale wanaomwogopa huruma kwa vizazi vyote.


Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.


Halafu mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kuume: ‘Mukuje, ninyi muliobarikiwa na Baba yangu; muingie katika Ufalme muliotayarishiwa tangu kuumbwa kwa dunia.


Inakupasa ushike neno la kwanza na la pili vilevile; maana anayemutii Mungu atayaepuka yote.


Aliishi maisha yake yote katika giza na huzuni, katika mahangaiko, magonjwa na hasira.


Wanaotenda zambi wanapatwa na hasara, lakini wenye haki wanafanikiwa.


atawabariki wote wanaomwabudu, atawabariki wakubwa kama vile wadogo.


Haleluia! Heri mutu anayemuheshimu Yawe, anayefurahia sana kushika amri zake.


Mumwabudu Yawe katika pahali pake patakatifu; tetemeka mbele yake, ee dunia nzima!


Ee dunia yote; tetemeka mbele yake! Ameweka ulimwengu imara, hautatikisika.


Hakuna mutu aliyekusudia kutenda maovu mbele ya Yawe kama Ahabu, ambaye alishawishiwa na Yezebeli, muke wake.


Musikule damu, nanyi mutafanikiwa pamoja na wazao wenu, maana mutakuwa munatenda kwa usawa mbele ya Yawe.


Basi, Mungu akawajalia mema wazalishaji wale, nao Waisraeli wakazidi kuongezeka na kuwa na nguvu sana.


Kwa hiyo mushike masharti yake na amri zake ambazo ninawapa leo kusudi mufanikiwe, ninyi pamoja na wazao wenu, na kuishi siku nyingi katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa ikuwe yenu milele.”


Mufanye angalisho kutii maneno haya niliyowaamuru, kusudi mupate kufanikiwa ninyi pamoja na wazao wenu nyuma yenu milele, maana mutakuwa munatenda mazuri na kwa usawa mbele ya Yawe, Mungu wenu.


Utapata matunda ya jasho lako, utafurahi na kupata uheri.


Usishangae ukiona katika inchi wamasikini wanagandamizwa, wananyimwa haki na sheria zao. Kila mwenye cheo anayewatesa wamasikini yupo chini ya mukubwa mwingine, na juu ya hao wote kuna wakubwa zaidi.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Sasa, kwa vile Mungu anazuia hasira yake, wala hajali sana makosa ya watu,


Heri mutu anayemwogopa Yawe siku zote, lakini mwenye moyo mugumu atapata hasara.


Mpaka hivi leo hamujajinyenyekeza wala kuogopa wala kuzifuata sheria zangu na masharti yangu nilizowawekea ninyi na babu zenu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite