Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 7:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mwisho wa jambo ni afazali kuliko mwanzo wake. Moyo muvumilivu ni bora kuliko moyo wa majivuno.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 7:8
20 Referans Kwoze  

Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.


Mutu asiyekuwa mwepesi wa hasira ana akili nyingi, lakini anayekasirika upesi anaongeza upumbafu.


Kwa sababu hiyo, mukuwe tayari kwa kutumikisha akili yenu. Mukeshe na muweke tumaini lenu lote katika baraka ile mutakayopewa wakati Yesu atakapotokea.


Tunawaita watu hao kuwa wenye heri, kwa sababu walivumilia. Mumekwisha kusikia habari za uvumilivu wa Yobu, na munajua namna Bwana alivyomutendea kwa mwisho. Maana Bwana anajaa huruma na wema.


Nanyi vilevile, muvumilie na kutia mioyo yenu nguvu, kwa maana Bwana yuko karibu kurudi.


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,


Lakini muendelee kuvumilia, maana kwa njia ile mutaokoa uzima wenu.”


Asiyekuwa mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwenye nguvu. Anayetawala nafsi yake ni bora kuliko anayetaka muji.


Mutu wa hasira mbaya anasababisha ugomvi, lakini asiyekuwa mwepesi wa hasira anautuliza.


Lakini Abrahamu akamujibu: ‘Mutoto wangu, kumbuka kwamba umekwisha kupewa mema yaliyokupasa wakati ulipoishi katika dunia, na Lazaro alipata taabu. Na sasa yeye anatulizwa, lakini wewe unateswa.


Muchoyo anachochea magomvi, lakini anayetegemea Yawe atafanikiwa.


Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.


Mukuwe wanyenyekevu kabisa, wapole na wavumilivu. Muvumiliane ninyi kwa ninyi kwa upendo.


Sifa nzuri ni bora kuliko marasi ya bei kali. Siku ya kufa ni bora kuliko siku ya kuzaliwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite