5 Afazali kusikia maonyo ya wenye hekima kuliko kusikiliza nyimbo za wapumbafu.
Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.
Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.
Umasikini na mazarau vinamupata yule asiyejali mafundisho, lakini mwenye kusikia maonyo anaheshimiwa.
Makaripio ya rafiki yanaonyesha uaminifu, lakini busu la adui ni udanganyifu.
Onyo kwa mwenye akili lina maana, kuliko mapigo mia moja kwa mupumbafu.
Anayezarau mashauri anajiletea maangamizi, lakini anayetii amri atapewa zawadi.
Usimwonye mwenye kiburi maana atakuchukia; umwonye mwenye hekima naye atakupenda.
Nilipovaa gunia kwa kuomboleza, nikageuka kuwa wimbo kwao.
Maana amri hizi ni taa, na shauri hilo ni mwangaza. Maonyo hayo ya mafundisho ni njia ya uzima.
Onyo la mwenye hekima kwa mutu musikilivu ni bora kuliko pete au ushanga wa zahabu safi.
Moyo wa mwenye hekima uko ndani ya nyumba ya kilio, lakini moyo wa mupumbafu unapenda raha.
Afazali kusikiliza maneno matulivu ya mwenye hekima, kuliko kusikiliza kelele za mufalme katika kikao cha wapumbafu.
Misemo ya wenye hekima ni kama fimbo ya kuongoza ngombe. Mezali zilizokusanywa pamoja na muchungaji mumoja ni kama misumari iliyopigiliwa kwa nguvu.