Nitawalewesha wakubwa na wenye hekima wake, watawala wake, maliwali na waaskari wake; watalala usingizi wa milele wala hawataweza tena kuamuka. –Ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi!
Wakiwa na hamu kubwa nitawatayarishia karamu: nitawalewesha mpaka wapepesuke; nao watalala usingizi wa siku zote na hawataamuka tena. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Basi, wakati wa saa sita za muchana, Beni-Hadadi na wale wafalme wenzake makumi tatu na wawili waliomwunga mukono walipokuwa katika mahema yao wakikunywa na kulewa, mashambulizi yakaanza.
Yule kijana alimwongoza Daudi mpaka kwenye kundi lile. Walipofika kule waliwakuta wanyanganyi wale wakiwa wametawanyika kila pahali maana walikuwa wakikula na kunywa kwa sababu vitu walivyonyanganya kutoka inchi ya Wafilistini na inchi ya Yuda vilikuwa vingi sana.
Abigaili aliporudi kwake, alimukuta Nabali akifanya karamu kubwa katika nyumba yake kama ya kifalme. Nabali alikuwa akifurahi sana ndani ya moyo maana alikuwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia neno lolote mpaka asubui.