Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 7:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Jambo moja nililotambua linalokuwa baya zaidi kuliko kifo, ni mwanamuke ambaye moyo wake ni mutego na wavu, na mikono yake ni kama minyororo. Lakini anayemupendeza Mungu anamwepuka mwanamuke yule, lakini mwenye zambi ananaswa naye.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 7:26
15 Referans Kwoze  

Kinywa cha mwasherati ni shimo refu; anayechukiwa na Yawe atatumbukia ndani yake.


Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Utaepukana na mwanamuke mwasherati, mwanamuke kahaba wa maneno matamu,


Lakini mujinga hajui kwamba mule muna wafu, wageni wa mwanamuke yule wako chini katika kuzimu.


Viongozi wa mufalme wakamwuliza: “Mutu huyu atatusumbua mpaka wakati gani? Uwaache watu hawa wajiendee wamutumikie Yawe, Mungu wao. Haujali kwamba inchi ya Misri inaangamia?”


Maana amri hizi ni taa, na shauri hilo ni mwangaza. Maonyo hayo ya mafundisho ni njia ya uzima.


Yatakulinda mbali na mwanamuke mubaya, yatakuepusha na maneno matamu ya mwanamuke mugeni.


Ninakuambia mimi Muhubiri, haya ndiyo niliyotambua nilipofanya uchunguzi wangu kidogokidogo.


Basi, usiku ule vilevile wakamulewesha baba yao kwa divai, kisha yule binti mudogo akakwenda akalala naye. Lakini baba yake hakujua wakati binti yake alipolala naye, wala wakati alipoondoka.


Hapa ndani ya nyumba yeye hana madaraka kuliko mimi. Yeye hakunikataza kushika chochote isipokuwa wewe tu kwa sababu wewe ni muke wake. Nitaweza namna gani basi kufanya uovu mubaya kama ule na kumukosea Mungu?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite