Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 6:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mungu anamujalia mutu utajiri, mali na heshima, hata hakosewi kitu chochote anachotamani, lakini hamupi uwezo wa kuvifurahia vitu hivyo. Pahali pake, mugeni fulani atavifaidia. Hayo nayo ni bure. Ni jambo la mateso mabaya.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 6:2
24 Referans Kwoze  

Na kwa kuwa Mungu amemuruhusu kuwa na furaha, mwanadamu hatakuwa na wasiwasi mwingi juu ya maisha yake mafupi.


Ee Yawe, mukono wako uwafukuze kati ya watu, tukio lao likuwe kutengana na wanaokuwa wazima. Uwashibishe kwa akiba uliyowawekea, watoto wao nao washibe na kuacha sehemu, wawaachie hata na wajukuu wao.


Mazarau yanatokana na unene wao; mioyo yao inatiririka mipango mibaya.


Vilevile, nitakupa yale ambayo haukuomba: nitakupa utajiri na heshima zaidi ya mufalme mwingine yeyote wa nyakati zako.


Inchi yetu imepewa kwa wageni, nyumba zetu kwa watu wengine.


Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Wageni wamenyonya nguvu zake, wala yeye mwenyewe hajui; imvi zimejaa juu ya kichwa chake, lakini yeye mwenyewe hana habari.


Ee mufalme, Mungu Mukubwa alimupa baba yako mufalme Nebukadneza ufalme, ukubwa, mamlaka na utukufu.


Aliishi maisha yake yote katika giza na huzuni, katika mahangaiko, magonjwa na hasira.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Tena nilitambua kwamba mutu anatoa jasho na kutumia ujuzi wake juu ya wivu tu kwa mwenzake. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Mungu akamujibu Solomono: “Kwa sababu jambo hili uliloomba liko ndani ya moyo wako, na wala haukuomba mali, wala utajiri, wala heshima wala haukuomba wanaokuchukia waangamizwe, wala maisha marefu, lakini umeomba hekima na maarifa kusudi uwatawale vizuri watu wangu ambao nimekupa ukuwe mufalme wao,


Alikufa akiwa muzee sana, alishiba siku, akiwa na mali na heshima. Mwana wake Solomono akakuwa mufalme kwa pahali pake.


Yawe akamupa Solomono sifa nzuri mbele ya Waisraeli wote, akamupa utukufu wa kifalme unaopita utukufu wa mufalme yeyote aliyeitawala inchi ya Israeli mbele yake.


Mutakapofika kule mutakuta watu wasiokuwa na wasiwasi wowote. Inchi hiyo ni kubwa, haikupungukiwa chochote, na Mungu ameitia katika mikono yetu.”


“Wageni wanaoishi katika inchi yenu watazidi kupata nguvu wakati ninyi mutazidi kufifia zaidi na zaidi.


“Taifa musilolijua litatwaa mazao yote ya inchi yenu na matunda ya jasho lenu, nanyi mutapondwa na kuteswa siku zote,


Kwa bahati mbaya, mali hiyo iliharibiwa katika matumizi mabaya. Kwa mwisho, mutu yule hakukuwa na kitu chochote wakati alipokuwa na mwana.


Mbona munatumia feza zenu kwa ajili ya kitu kisichokuwa chakula? Kwa nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha? Munisikilize mimi kwa uangalifu, nanyi mutakula vinavyokuwa vitamu, na kufurahia vinavyokuwa bora.


Kama Mungu anamupa mutu utajiri na mali na kumujalia wakati wa kuyafurahia, basi mwanadamu ashukuru na avifaidie hivyo alivyojipatia kwa jasho lake. Hiyo ni zawadi kutoka kwa Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite