Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 6:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Nani anayejua yanayofaa kwa mutu katika maisha haya mafupi yasiyokuwa na faida, maisha ambayo yanapita kama kivuli? Nani anayejua yale yatakayotukia chini ya jua nyuma ya kufa kwake?

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 6:12
28 Referans Kwoze  

Ninyi hamujui namna gani maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Kwa maana ninyi ni kama muvuke unaoonekana kwa wakati kidogo, kisha unatoweka.


Basi, nikatambua kwamba hakuna jambo linalokuwa bora zaidi kwa mwanadamu kufanya kuliko kufurahia kazi yake, kwa sababu amepangiwa hivyo. Nani anayeweza kumujulisha mwanadamu yale yatakayokuwa kisha kufa kwake?


Anachanua kama maua, kisha ananyauka. Anakimbia kama kivuli na kutoweka.


Mwanadamu ni kama pumzi tu; siku zake zinapita kama kivuli.


Lakini hakuna furaha kwa waovu. Wao watapita kama kivuli, maisha yao hayatakuwa marefu kwa sababu hawamwogopi Mungu.


Hajui ni kitu gani kitakachotukia nyuma, maana ni nani anayeweza kumujulisha yatakayotukia nyuma?


Sisi ni watu wa juzijuzi tu, hatujui kitu; siku zetu katika dunia ni kivuli kinachopita.


Sisi tuko wageni mbele yako, na wasafiri kama vile babu zetu walivyokuwa wote. Siku zetu katika dunia ni kama kivuli kinachopita, hapa hakuna tumaini la kukaa.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Upendo wao, chuki zao na tamaa zao, vyote vimetoweka pamoja nao, wala hawatashiriki tena katika kitu chochote hapa chini ya jua.


Nilitafuta kwa hekima namna ya kujichangamusha mwili kwa divai na kutenda sawa na wapumbafu. Nilitaka kuona kitu gani ni kizuri kwa wanadamu kufanya wanapoishi maisha yao mafupi hapa chini ya mbingu.


Ninatoweka kama kivuli cha magaribi; nimepeperushwa kama nzige.


kwa sababu ya kasirani na hasira yako, maana umeniokota na kunitupilia mbali.


Lakini mimi nitauona uso wako, maana mimi ni mutu wa haki; nitakapoamuka nitajaa furaha kwa sababu unanitokea.


Mutoe sadaka zinazokuwa sawa, na kumutumainia Yawe.


Watoto wake wakiheshimika, yeye hana habari. Wakizarauliwa, yeye haoni kabisa.


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Ee Yawe, utajificha hata milele? Mpaka wakati gani hasira yako itawaka kama moto?


Ametuwezesha kuwashinda watu wa mataifa, ameyaweka mataifa chini ya mamlaka yetu.


Wewe, ee Yawe, ndiwe riziki yangu kubwa, majaliwa yangu yako katika mikono yako.


Hakuna kitu kizuri kwa mwanadamu, isipokuwa kula na kunywa na kufurahia matunda ya jasho yake. Hili nalo nimeliona kwamba linatoka kwa Mungu,


Maneno yanapokuwa mengi, ndivyo yanaendelea kuwa bure. Hayana faida.


Katika maisha yangu ya bure, niliona kila kitu. Mutu wa haki anakufa ingawa ni wa haki, ambapo mutu mwovu anaendelea kuishi maisha marefu ingawa ni mwovu.


Furahia maisha pamoja na muke wako unayemupenda muda wote wa maisha yako ya bure ambayo Mungu amekujalia hapa chini ya jua, maana hilo ndilo ulilopangiwa katika maisha, katika kutoa jasho yako hapa chini ya jua.


Mupumbafu anasema maneno mengi. Mwanadamu hajui yatakayokuwa, wala yale yatakayotukia nyuma yake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite