Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 6:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kila kitu kinachotukia kilikwisha kupangwa tangu zamani. Hali ya mwanadamu inajulikana, na tunajua kwamba muzaifu hawezi kubishana na mutu mwenye nguvu zaidi.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 6:10
18 Referans Kwoze  

Mungu si mutu kama mimi nipate kumujibu, hata tuweze kwenda katika tribinali pamoja.


Wewe mwenye kuchunguza makosa utashindana na Mungu Mwenye Uwezo? Wewe unayebishana nami Mungu, basi ujibu mambo hayo!


Kama vile simba anavyochomoka kutoka ndani ya vichaka vya muto Yordani na kuingia kwenye mbuga, ndivyo nitakavyowafukuza kwa rafla Waedomu toka katika inchi yao. Nami nitamuweka huko mutawala yeyote nitakayemuchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani anayeweza kunishitaki? Ni muchungaji gani anayeweza kunipinga?


Kinachotukia sasa, kilikwisha tukia; kitakachotukia nyuma kilikwisha kutukia. Mungu anafanya kitu kitukie tena na tena.


Kwa nini unashindana naye, ukisema hatajibu ulizo lako moja?


Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Maisha ya mwanadamu ni kama majani tu, yanachanua kama maua:


Lakini Yawe Mungu akamwita yule mwanaume: “Uko wapi?”


Au tunataka kumuchokoza Bwana hata asikie wivu? Munafikiri kuwa sisi tuko na nguvu kuliko yeye?


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Maneno yanapokuwa mengi, ndivyo yanaendelea kuwa bure. Hayana faida.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite