Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 5:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Faida ya mavuno ya inchi ni kwa watu wote, hata mufalme vilevile anatumainia mavuno yale.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 5:8
60 Referans Kwoze  

Kisha nikaona mateso yote yanayofanyika chini ya jua. Watu wanaogandamizwa wanalia machozi, lakini hakuna mutu yeyote anayewafariji. Wagandamizaji wao wana nguvu, ndiyo sababu hakuna wa kuwafariji.


Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”


Zaidi ya hayo, nimegundua chini ya jua kwamba uovu unatawala kwa pahali pa haki na sheria.


Zaburi ya Asafu. Mungu anasimamia baraza lake. Anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu:


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.


Na wewe, mutoto wangu, utaitwa nabii wa Mungu Mukubwa, maana utatangulia mbele ya kufika kwa Bwana, kusudi umutengenezee njia.


Malaika akamujibu: “Roho Mutakatifu atakufikia, na uwezo wa Mungu Mukubwa utakufunika kama vile kivuli. Kwa sababu hii mutoto yule atakayezaliwa ataitwa Mutakatifu na Mwana wa Mungu.


Yeye atakuwa mwenye mamlaka, na ataitwa Mwana wa Mungu Mukubwa. Bwana Mungu atamuweka kuwa mutawala wa ufalme wa babu yake Daudi.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Kwa watu hawa waliobaki, hali hii inaonekana kuwa kitu kisichowezekana; lakini munazani haiwezekani kwangu mimi? –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Munawafukuza wake za watu wangu kutoka nyumba zao nzuri. Mumewaondolea watoto wao utukufu wangu milele.


Farasi wanaweza kukimbia katika mawe makubwa? Watu wanaweza kulima bahari na ngombe? Lakini ninyi mumeigeuza sheria kuwa sumu, na tunda la haki kuwa uchungu.


Maana mimi ninajua wingi wa makosa yenu na ukubwa wa zambi zenu; ninyi munawatesa watu wema, munapokea kituliro na kuzuia wakosefu wasipate haki katika tribinali.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Wakati Yawe atakapomaliza kazi zake zote kwenye mulima Sayuni na katika Yerusalema, atamwazibu mufalme wa Asuria, kwa sababu ya majivuno na kiburi chake.


Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!


Muna haki gani kuwagandamiza watu wangu, na kuwatendea wamasikini vibaya? –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.


Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.


Maana Yawe ni Mungu mukubwa; yeye ni mufalme mukubwa juu ya miungu yote.


Wafezeheke na kuhangaika milele, waangamie kwa haya kabisa.


ningekimbilia pahali penye usalama, mbali na upepo mukali na zoruba.”


Basi wandugu zangu, musishangae kama watu wa dunia hii wakiwachukia ninyi.


Wandugu wapendwa, musishangae kwa kuona mateso makubwa ya kuwajaribu munayopata. Musiyahesabu kuwa kitu kigeni kwenu.


Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!


Anayemutesa masikini kwa kujitajirisha na anayewapa watajiri zawadi, wote wawili wataishia kuwa wamasikini.


Usiseme kisha: “Hatukujua!” Maana Mungu anayepima mioyo ya watu anaona; yeye atakulipa kulingana na matendo yako!


Yule anayependa feza hatatosheka na feza, wala anayetamani mali hata akiipata hatatosheka. Hayo nayo ni bure.


Mwenye hekima akimutesa mutu, yeye anafanya kama mupumbafu. Kupokea kituliro kunapotosha akili.


Haya yote nimeyaona katika uchunguzi wangu juu ya yote yanayotendeka hapa chini ya jua, ambako mwanadamu anatawala mwenzake na kumutesa.


Lakini baba yake, kwa sababu alilipisha bei isiyokuwa ya haki na kumwibia ndugu yake, wala hakuwatendea wandugu zake vizuri, hakika atakufa kwa sababu ya uovu wake.


Hata katika jangwa vilevile alijenga minara, akachimba visima vingi, maana alikuwa na makundi mengi ya nyama kwenye sehemu za miinuko na mabonde. Alikuwa na walimaji na watunza mizabibu kwenye milima, na katika inchi yenye mboleo maana alipenda mulimo.


Anawaacha waovu wajione salama, lakini macho yake yanachunguza mienendo yao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite