Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 5:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Usishangae ukiona katika inchi wamasikini wanagandamizwa, wananyimwa haki na sheria zao. Kila mwenye cheo anayewatesa wamasikini yupo chini ya mukubwa mwingine, na juu ya hao wote kuna wakubwa zaidi.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 5:7
11 Referans Kwoze  

“Ninawaambia wazi kwamba kwa Siku ya hukumu, watu watasamba kila neno lisilokuwa na maana walilosema.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Wenye zambi wanatenda maovu mara mia. Hata hivyo, wanaendelea kuishi. Lakini, mimi ninajua kwamba itakuwa heri kwa wanaomwogopa Mungu, kwa sababu ya woga wao.


Ukimutolea Mungu ahadi, usikawie kuitimiza. Mungu hapendezwi na wapumbafu. Timiza kile ulichoahidi.


Ninajua kwamba jambo lolote Mungu analotenda linadumu milele. Hakuna kinachoweza kuongezwa wala kupunguzwa. Mungu amefanya mambo yakuwe hivyo kusudi wanadamu wamwogope yeye.


Moyo wako usiwaonee wivu wenye zambi, lakini endelea kumwogopa Yawe siku zote.


Inakupasa ushike neno la kwanza na la pili vilevile; maana anayemutii Mungu atayaepuka yote.


Lakini hakuna furaha kwa waovu. Wao watapita kama kivuli, maisha yao hayatakuwa marefu kwa sababu hawamwogopi Mungu.


Zaidi ya hayo, nimegundua chini ya jua kwamba uovu unatawala kwa pahali pa haki na sheria.


Haya yote nimeyaona katika uchunguzi wangu juu ya yote yanayotendeka hapa chini ya jua, ambako mwanadamu anatawala mwenzake na kumutesa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite