Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 5:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kwa bahati mbaya, mali hiyo iliharibiwa katika matumizi mabaya. Kwa mwisho, mutu yule hakukuwa na kitu chochote wakati alipokuwa na mwana.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 5:13
29 Referans Kwoze  

Basi, Loti akawaendea wachumba wa wabinti zake, akawaambia: “Haraka! Mutoke pahali hapa, maana Yawe atauangamiza muji huu.” Lakini wao wakamwona kama mutu mwenye kuchekesha tu.


“Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyezoea kuvaa nguo zenye kuwa laini sana za bei kali zaidi na aliyeishi katika raha siku zote.


Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.


Haya yote nimeyaona katika uchunguzi wangu juu ya yote yanayotendeka hapa chini ya jua, ambako mwanadamu anatawala mwenzake na kumutesa.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.


Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao, wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.


Ndizo njia za wanyanganyi; maisha yao yananyanganywa.


Basi, Abramu akakomboa mali yote iliyonyanganywa na waadui, na kumukomboa mwipwa wake Loti, mali yake, pamoja na wanawake na watu wengine.


Lakini Zakayo akasimama mbele ya Bwana na kumwambia: “Bwana! Ninawapa masikini nusu ya mali zangu, na kama nimetwaa kitu cha mutu kwa kumudanganya, nitamurudishia mara ine sawa na kitu kile.”


Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo sanamu za feza na zahabu walizojitengenezea kusudi waziabudu.


Lakini muke wa Loti aliyekuwa nyuma ya Loti, akatazama nyuma, akageuka nguzo ya chumvi.


Kwa vile ulafi wake hauna mwisho, hataweza kuokoa kitu chochote cha lazima.


Kama vile mwanadamu alivyokuja katika dunia akiwa uchi toka katika tumbo la mama yake, ndivyo atakavyorudi uchi kule alikotoka. Hataweza kupeleka hata sehemu ndogo ya mapato ya kazi yake.


Usijichokeshe na kutafuta utajiri; acha kufikiri juu yake.


Maana utajiri haudumu milele, wala taji haidumu kwa vizazi vyote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite