Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 5:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Usingizi wa mutumishi ni mutamu, akuwe ameshiba au amekula kidogo tu. Lakini usingizi wa tajiri ni wa wasiwasi siku zote, maana mali yake inamuzuia kupata usingizi.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 5:11
16 Referans Kwoze  

Kwa maana kila kitu kinachokuwa katika dunia, kama vile tamaa ya kimwili, tamaa ya macho, na majivuno ya maisha, hivi vyote havitoki kwa Baba, lakini vinatoka katika dunia.


Yawe wa majeshi anasababisha juhudi za watu zipotelee katika moto, na mataifa yajishugulishe bure.


Macho yako yatakapokuwa yanaanza tu kuuona, nao utatoweka mara moja. Maana hakika utajiri unaota mabawa, unaruka na kutoweka katika anga kama tai.


Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kumata upepo. Afazali kufurahia kitu ambacho uko nacho kuliko kuhangaika kwa kutamani kitu kingine.


Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.


Wakati ule, Abramu alikuwa ametajirika sana. Alikuwa na makundi ya nyama, feza na zahabu.


Naye akamutendea Abramu mema kwa ajili ya Sarai. Akamupa kondoo, ngombe, punda dume, watumishi na wajakazi, punda dike na ngamia.


Mutu anayepata mali isiyokuwa ya usawa ni kama kwale anayelalia mayai ambayo hakutaga. Mali yanamwishia angali kijana, na kwa mwisho anageuka sawa mupumbafu.


Nikakuwa mukubwa, mukubwa kuwapita wote waliopata kuwa katika Yerusalema mbele yangu. Na hekima yangu ikakaa ndani yangu.


Tena, nimeona jambo moja ovu sana chini ya jua: mutu alijikusanyia mali, ikakuwa hatari kwake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite