Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 3:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 wakati wa kupasua na wakati wa kushona, wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema,

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 3:7
32 Referans Kwoze  

Usimwaminie mwenzako, wala usimutumainie rafiki yako. Chunga mudomo wako, usimwambie kitu muke wako wewe mwenyewe.


Basi, kutakuwa wakati mubaya ambao hata mwenye hekima atanyamaza.


Kwa maana sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo tuliyoyaona na kuyasikia.”


Heri kwa mutu kukaa peke yake na kimya, mambo mazito yanapomupata kutoka kwa Mungu.


Munapasua nguo zenu kwa kuonyesha huzuni, lakini inafaa mioyo yenu ipasuke vilevile. Murudilie Yawe, Mungu wenu. Yeye amejaa huruma na rehema, hakasiriki upesi, ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia zake kusudi asiazibu.


Maana, mimi na watu wangu tumeuzishwa kusudi tuuawe, tuangamizwe na kuteketezwa kabisa. Kama tungeuzishwa tu kuwa watumwa na wajakazi, ningekaa kimya wala nisingekusumbua. Ingawa tutateswa hakuna adui atakayeweza kulipa hasara hii kwa mufalme.”


Siku hiyo, nyimbo za nyumba ya kifalme zitakuwa maombolezo. –Ni ujumbe wa Yawe.– Kutakuwa maiti nyingi, nazo zitatupwa fasi zote kimyakimya.


Watu wanauliza: Kwa nini sisi tunakaa tu hapa? Tukusanyike, tuingie katika miji yenye kuzungukwa na kuta, tuangamie kule! Yawe, Mungu wetu, amekusudia tuangamie, ametupa maji yenye sumu tukunywe, kwa sababu tumemukosea yeye.


Lakini watu walinyamaza, wala hawakumujibu neno kama vile walivyoamuriwa na mufalme akisema: “Musimujibu.”


Nilisema: “Nitayachunga maisha yangu, kusudi nisitende zambi kwa usemi wangu. Nitafunga midomo yangu waovu wanapokuwa karibu nami.”


Mara mufalme aliposikia maneno ya mwanamuke yule alipasua nguo zake kwa huzuni, na watu waliokuwa karibu na ukuta waliona kwamba alikuwa amevaa nguo ya gunia ndani yake.


Mufalme wa Israeli aliposoma barua hii alipasua nguo yake na kusema: “Sababu gani mufalme wa Aramu anataka nimuponyeshe mutu huyu ukoma wake? Anafikiri kwamba mimi ni Mungu anayekuwa na uwezo wa kuua au kufufua? Mufahamu basi, muone kwamba mutu huyu anataka kuniletea ugomvi!”


Lakini, Ahabu aliposikia maneno hayo, akapasua nguo zake, akavaa gunia peke yake, akafunga, akakuwa analala na gunia, na kwenda huko na huko kwa huzuni.


Kisha, mufalme Daudi akamwambia Yoabu na wale wote waliokuwa pamoja naye, wapasue nguo zao, wavae nguo ya gunia kusudi wafanye kilio kwa ajili ya Abeneri. Wakati wa mazishi hayo, mufalme Daudi alitembea nyuma ya kipoyi cha maiti ya Abeneri.


Daudi akapasua nguo yake kwa huzuni. Hata watu waliokuwa pamoja na Daudi wakafanya vilevile.


Nitaweza namna gani kumurudilia baba yangu bila kijana huyu? Siwezi kuvumilia kuona hasara itakayomupata baba yangu.”


Halafu Yuda akamukaribia Yosefu na kumwambia: “Bwana, ninakuomba uniruhusu mimi mutumishi wako, nijitetee mbele yako kwa maneno machache. Ninakusihi usinikasirikie, maana wewe ni kama mufalme wa Misri mwenyewe.


Halafu Yakobo akararua nguo zake kwa huzuni, akavaa nguo ya gunia katika kiuno. Akamulilia mwana wake kwa muda wa siku nyingi.


Basi, Rubeni aliporudi kwenye lile shimo, hakumwona Yosefu tena, kwa hiyo akararua nguo zake kwa huzuni,


Mara moja Petro akaenda pamoja nao. Naye alipofika wakamupeleka ndani ya chumba cha gorofi. Wajane wote wakamuzunguka Petro, wakilia na kumwonyesha kanzu na nguo zote Dorika alizowashonea wakati alipokuwa angali muzima.


Lakini, ingawa mufalme na watumishi wake wote waliyasikia maneno hayo yote, hawakuogopa wala kurarua nguo zao kwa huzuni.


Kisha wakaikaa kwenye udongo pamoja na Yobu kwa siku saba, muchana na usiku, bila kumwambia neno lolote maana waliona mateso yake kuwa makubwa sana.


wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuchunga na wakati wa kutupa,


Saulo akajibu: “Alituambia waziwazi kwamba punda wamepatikana.” Lakini Saulo hakumwelezea kwamba Samweli alimwambia kwamba atakuwa mufalme.


Lakini watu walinyamaza, wala hawakumujibu neno kama vile walivyoamuriwa na mufalme akisema: “Musimujibu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite