Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 3:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Ninajua kwamba jambo lolote Mungu analotenda linadumu milele. Hakuna kinachoweza kuongezwa wala kupunguzwa. Mungu amefanya mambo yakuwe hivyo kusudi wanadamu wamwogope yeye.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 3:14
30 Referans Kwoze  

Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Mipango ya Yawe inadumu milele; kusudi lake linadumu kwa vizazi vyote.


Kwa maana vitu vyote vinatoka kwake, navyo viko kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Atukuzwe hata milele! Amina.


Lakini ikiwa vimeanzishwa na Mungu, hamutaweza kuwazuiza. Basi mujiangalie vizuri musikuje kuonekana kuwa munapigana na Mungu!”


Usiongeze neno katika maneno yake, kusudi asikukaripie, nawe usionekane kuwa mwongo.


Na kwa njia hiyo watapata tumaini la uzima wa milele, ambalo Mungu asiyesema uongo alituahidi mbele ya mwanzo wa nyakati.


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Mungu amefanya hivi kufuatana na kusudi lake la milele alilofanya kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.


Hivi walitimiza mambo uliyokuwa umekusudia tangu zamani kwa uwezo wako na kwa mapenzi yako.


Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.


Nilitangaza mambo ya mwisho tangu mwanzo, tangu zamani nilitangaza mambo yatakayotukia. Kusudio langu litatimia; mimi nitatimiza nia yangu yote.


Inakupasa ushike neno la kwanza na la pili vilevile; maana anayemutii Mungu atayaepuka yote.


Usishangae ukiona katika inchi wamasikini wanagandamizwa, wananyimwa haki na sheria zao. Kila mwenye cheo anayewatesa wamasikini yupo chini ya mukubwa mwingine, na juu ya hao wote kuna wakubwa zaidi.


Katika moyo wa mutu muna mipango mingi, lakini anachokusudia Yawe ndicho kitakachokamilika.


wakati ulipoinuka kutimiza hukumu, kuwaokoa wote wanaoteswa katika dunia.


Atawaangamiza kwa sababu ya maneno yao; kila atakayewaona atatikisa kichwa.


Ewe Bwana, hakuna asiyekuogopa, wala hakuna asiyekutukuza, kwa maana wewe peke yako ndiwe mutakatifu. Mataifa yote yatakuja kukuabudu, kwa maana matendo yako ya haki yameonyeshwa wazi.”


Kwa hiyo yule beberu alijitukuza sana. Lakini alipofikia kilele cha nguvu zake, ile pembe yake kubwa ikavunjika. Pahali pake kukaota pembe ine zilizoonekana waziwazi, zikiwa zimeelekea pande ine za dunia.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Yawe ni mulima wa usalama. Kazi zake ni kamilifu, njia zake zote ni za haki. Yeye ni Mungu mwaminifu asiyekuwa na kosa, yeye anafanya mambo ya usawa na ya haki.


Matendo ya Mungu ni makamilifu. Ahadi ya Yawe ni ya kuaminika. Yeye ni ngao kwa wote wanaomukimbilia.


Ndoto zikizidi, kuna maangamizi na maneno yanakuwa mengi. Jambo la maana ni kumwogopa Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite