Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 3:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kama mwanadamu anakula na kunywa na kufurahia matunda ya jasho yake, hayo ni majaliwa ya Mungu.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 3:13
14 Referans Kwoze  

Kwenda ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo wenye kuchangamuka, maana Mungu amekwisha kukubali kazi yako.


Hakuna kitu kizuri kwa mwanadamu, isipokuwa kula na kunywa na kufurahia matunda ya jasho yake. Hili nalo nimeliona kwamba linatoka kwa Mungu,


Utapata matunda ya jasho lako, utafurahi na kupata uheri.


Mungu anamujalia mutu utajiri, mali na heshima, hata hakosewi kitu chochote anachotamani, lakini hamupi uwezo wa kuvifurahia vitu hivyo. Pahali pake, mugeni fulani atavifaidia. Hayo nayo ni bure. Ni jambo la mateso mabaya.


Huko, mutakula mbele ya Yawe, Mungu wenu, na mutafurahi ninyi pamoja na watu wa nyumba zenu kwa ajili ya mafanikio yenu Yawe, Mungu wenu, aliyowabarikia.


Nawe utafurahia mema yote ambayo Yawe, Mungu wako, amekujalia wewe na jamaa yako. Nao watafurahi pamoja nawe.


Mukuje, enyi vijana munisikilize, nami nitawafundisha kumwabudu Yawe.


Nilitafuta kwa hekima namna ya kujichangamusha mwili kwa divai na kutenda sawa na wapumbafu. Nilitaka kuona kitu gani ni kizuri kwa wanadamu kufanya wanapoishi maisha yao mafupi hapa chini ya mbingu.


Basi, mimi ninasifu furaha, kwa maana hapa chini ya jua hakuna kitu kinachokuwa kizuri zaidi kuliko kula na kunywa na kujifurahisha. Haya ndiyo mutu anayoweza kufanya anapotoa jasho katika muda wa maisha yake aliyojaliwa na Mungu chini ya jua.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite