Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Nilijikusanyia feza na zahabu kutoka hazina za wafalme na toka katika majimbo, nami nilipata waimbaji wanaume na wanawake, na wahabara wanaotamaniwa.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 2:8
21 Referans Kwoze  

Kisha malkia akamupa mufalme zaidi ya kilo elfu ine za zahabu, marasi nyingi sana na mawe ya bei kali. Hakuna aliyeweza hata kidogo kumuletea mufalme Solomono marasi mengi sana sawa yale malkia wa Seba aliyomuletea.


Walisafiri kwenda katika inchi ya Ofiri, na kuleta toka kule zahabu, wakamuletea mufalme Solomono yapata kilo elfu kumi na ine.


Lakini Barzilayi akamwambia mufalme: “Niko tena na miaka mingi ya kuishi ndipo niende nawe mufalme mpaka Yerusalema?


Kila mwaka, Solomono alipelekewa zahabu kilo elfu makumi mbili na mbili.


Ninyi munapenda kuimba ovyo na sauti ya vinubi na kutunga ala mupya za muziki mukimwiga mufalme Daudi.


Basi, mutakaposikia tena sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, muko tayari kuinama chini na kuiabudu sanamu niliyotengeneza? Kama mukikataa, mutatupwa mara moja katika furu la moto mukali. Ni mungu gani anayeweza kuwaokoa katika mikono yangu?


Kwa hiyo, watu wote, mara tu waliposikia sauti za baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, walianguka uso mpaka chini na kuiabudu ile sanamu ya zahabu ambayo mufalme Nebukadneza alisimamisha.


mukisikia sauti ya baragumu, filimbi, kinubi, zeze, santuri, zomari na sauti za ala nyingine za muziki, munapaswa kuinama chini na kuabudu sanamu ya zahabu mufalme Nebukadneza aliyosimamisha.


Solomono alitumia miti hiyo kwa kutengeneza madari ya nyumba ya Yawe na nyumba ya kifalme, na tena kwa kutengeneza vinubi na vinanda vya waimbaji. Mpaka wakati ule miti hiyo ilikuwa haijaonekana katika inchi ya Yuda.


Wana wake wote walipiga muziki kwa matoazi, vinanda na vinubi, kwenye ibada katika nyumba ya Yawe wakiwa chini ya uongozi wa baba yao. Asafu, Yedutuni na Hemani walikuwa chini ya uongozi wa mufalme.


Mufalme Daudi na viongozi wa Walawi, wakachagua wazao wa Asafu, wa Hemani, na wa Yedutuni, kwa kuongoza katika kazi ya kutabiri kwa kutumia vinubi, na vinanda na matoazi. Haya ndiyo majina ya wale waliochaguliwa kwa kuongoza ibada, pamoja na aina ya kazi iliyofanywa na kila kikundi:


Pahali pa ngao hizo, mufalme Rehoboamu alitengeneza ngao za shaba na kuziweka chini ya ulinzi wa wachungaji wa mulango wa nyumba ya kifalme.


Vyombo vyote vya kunywa divai vya mufalme Solomono vilikuwa vya zahabu, na vyombo vyote vilivyokuwa katika Nyumba ya Pori ya Lebanoni vilikuwa vya zahabu safi; hakuna kilichotengenezwa kwa feza maana madini ya feza haikuhesabiwa kuwa kitu wakati ule.


Hiramu alikuwa amemupelekea mufalme Solomono zahabu kilo elfu tatu na mia sita.


Solomono akakuwa na wanawake mia saba, wote wabinti wa kifalme, na wahabara mia tatu. Hao wanawake wakamupotosha.


Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite