Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 2:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Mutu anafaidia nini kutokana na jasho yake yote, na juhudi anazohangaika nazo chini ya jua?

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 2:22
21 Referans Kwoze  

Mwanadamu anafaidia nini kwa jasho lake lote hapa chini ya jua?


Munajisumbua bure kuamuka asubui mapema na kuchelewa kwenda kupumzika magaribi, mujipatie chakula kwa jasho lenu. Mungu anatimiza mahitaji ya wapendwa wake hata wanapolala.


Mumutolee masumbuko yenu yote kwa maana yeye anawashugulikia.


Basi kama tukiwa na chakula na nguo, vile vinatosha.


Musijisumbue juu ya neno lolote, lakini katika kila neno mutoe mahitaji yenu kwa Mungu, mukimwomba, mukimusihi na kumushukuru.


Basi musijisumbue kwa ajili ya kesho, kwa maana kesho itajisumbukia yenyewe. Kila siku ina masumbuko yake inayoitoshelea.


Ni afazali kuwa na kidogo tu, pamoja na amani ndani ya moyo, kuliko kutoa jasho kwa ajili ya kukamata upepo.


Mufanya kazi anafaidia nini kutokana na jasho aliyotoa?


Ni faida gani kwa mutu kupata utajiri wote wa dunia, lakini anapoteza uzima wake? Hakuna kitu mutu anachoweza kutoa kwa kukomboa uzima wake.


Utupe chakula chetu cha kila siku.


Basi, mimi ninasifu furaha, kwa maana hapa chini ya jua hakuna kitu kinachokuwa kizuri zaidi kuliko kula na kunywa na kujifurahisha. Haya ndiyo mutu anayoweza kufanya anapotoa jasho katika muda wa maisha yake aliyojaliwa na Mungu chini ya jua.


Basi, haya ndiyo niliyotambua: jambo zuri na lenye kufaa kwa mwanadamu ni kula, kunywa na kufurahia matunda ya jasho anayotoa hapa chini ya jua, siku zile chache za maisha aliyojaliwa na Mungu, maana hivi ndivyo alivyopangiwa.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Basi musijisumbue kwa kutafuta chakula au kinywaji.


Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ni kwa sababu hii ninawaambia: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwamba mutakula nini; wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu, kwamba mutavaa nini.


“Ni kwa sababu hii ninawaambia ninyi: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwa ajili ya chakula au kwa ajili ya kinywaji, wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu kwamba mutavaa nini. Uzima ni wa lazima kuliko vyakula, nao mwili ni wa lazima kuliko nguo.


Njaa inamusukuma mutu kufanya kazi, maana tamaa ya kinywa chake inamupa bidii.


mukubali kuongozwa na watu kama hawa na wale wote wanaotumika na bidii pamoja nao.


Kisha nikafikiri juu ya yote niliyokuwa nimefanya kwa mikono yangu, na jinsi nilivyotoa jasho kwa kuyafanya. Nikatambua kwamba yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo. Hakukukuwa faida yoyote chini ya jua.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite