Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 2:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Maana, wakati mwingine, mutu ambaye amefanya kazi kwa kutumia hekima, akili na maarifa yake, anamwachia mutu mwingine afurahie matunda ya kazi ambayo hakuitoshea jasho. Hayo nayo ni bure. Ni jambo baya sana.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 2:21
15 Referans Kwoze  

Lakini macho yako wewe na moyo wako, vinaelekea tu mapato yasiyokuwa ya haki. Unamwanga damu ya wasiokuwa na kosa, nawe unawatesa watu na kuwatendea kwa ukali.


Unazani umekuwa mufalme kwa kujenga na mierezi? Baba yako alikula na kunywa, alifuata sheria yangu na kutenda mambo ya haki, na mambo yake yaliendeka vizuri.


Kuwa na hekima ni bora kuliko kutegemea silaha, lakini mwenye zambi mumoja anaharibu mazuri mengi.


Pasaka kama hiyo ilikuwa haikufanyika katika Israeli yote tangu siku za nabii Samweli. Hakujatokea mufalme hata mumoja wa Israeli aliyefanya Pasaka kama hii iliyofanyika na mufalme Yosia, makuhani, Walawi na watu wote wa inchi ya Yuda, wa Israeli vilevile na wakaaji wa Yerusalema.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe. Alifuata njia za Daudi babu yake, na kushika amri za Yawe kwa uangalifu.


kimwezeshe aendelee kuishi siku zote, bila kuona kaburi.


Basi, nilipofikiri tena juu ya jasho yote niliyotoa chini ya jua, nilikata tamaa.


Tena nilitambua kwamba mutu anatoa jasho na kutumia ujuzi wake juu ya wivu tu kwa mwenzake. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Kweli, kila mutu anapita kama kivuli; masumbuko yake yote ni bure tu; anakusanya mali, hajui atakayeipata!


Inaonekana wazi kuwa hata wenye hekima wanakufa, nao wapumbafu na wajinga vilevile. Wote wanawaachia wengine mali zao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite