Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 12:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 12:8
10 Referans Kwoze  

Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure!


Hakuna mutu anayekuwa na uwezo wa kushikilia roho yake kusudi asikufe; hakuna mutu anayekuwa na uwezo juu ya siku ya kufa. Wakati wa vita hakuna kuponyoka, na uovu hauwezi kumwokoa mwovu.


Nani anayejua yanayofaa kwa mutu katika maisha haya mafupi yasiyokuwa na faida, maisha ambayo yanapita kama kivuli? Nani anayejua yale yatakayotukia chini ya jua nyuma ya kufa kwake?


Tena nilitambua kwamba mutu anatoa jasho na kutumia ujuzi wake juu ya wivu tu kwa mwenzake. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Kwa hiyo, nikachukia maisha, maana yote yanayotendeka chini ya jua yalinisikitisha. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Nimeyaona mambo yote yanayofanywa chini ya jua. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo!


Enyi watu, mutumainie Mungu siku zote; mumufungulie yanayokuwa ndani ya moyo wenu. Yeye ndiye kimbilio letu.


Maneno haya ni ya Muhubiri mwana wa Daudi, aliyekuwa mufalme kule Yerusalema.


Mimi Muhubiri, nilikuwa mufalme wa Israeli, kule Yerusalema.


Nilifanya bidii kujua umbalimbali kati ya hekima, wazimu na upumbafu. Lakini niligundua kwamba kufanya hivyo ni sawa na kutaka kukamata upepo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite