Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Muhubiri 12:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 mavumbi yanarudilia inchi tena, na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.

Gade chapit la Kopi




Muhubiri 12:7
23 Referans Kwoze  

Wengi wa wale ambao wamekwisha kufa, watafufuka; wengine watapata uzima wa milele, na wengine watapata haya na kuzarauliwa milele.


Mwanadamu akitoa pumzi yake ya mwisho, anarudi katika mavumbi alimotoka, na hapo mipango yake yote inatoweka.


Ujumbe wa Yawe unaoelekea Israeli. Yawe aliyezitandaza mbingu, aliyeiweka misingi ya dunia na kumupa mwanadamu uzima anasema hivi:


Kwa jasho la uso wako utajipatia chakula, mpaka utakaporudi katika udongo, maana ulitwaliwa katika udongo. Wewe ni mavumbi na utarudi katika mavumbi.”


Halafu Yawe Mungu akamwumba mwanaume kwa udongo, akamupulizia ndani ya pua pumzi ya uzima, na yule mwanaume akakuwa kiumbe chenye uzima.


Maana sitaendelea kugombana wala kuwakasirikia siku zote, maana hao niliowaumba watazimia mbele yangu, nami ndiye niliyewapa pumzi yangu ya uzima.


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Unawarudisha watu katika mavumbi walimotoka, ukisema: “Wanadamu, murudi!”


Japo alijisikia amejaa nguvu ya ujana, lakini italala pamoja naye katika mavumbi.


Ee Yawe, Mungu unayekuwa asili ya uzima wote, ninakuomba umuchague mutu wa kusimamia watu hawa,


Lakini ninyi mumefikia kwenye mukutano wa furaha wa wazaliwa wa kwanza wa Mungu walioandikwa majina zao katika mbingu. Mumefikia vilevile karibu na Mungu, anayekuwa mwamuzi wa watu wote na kwenye nafsi kunapokuwa roho za watu wenye haki waliofanywa kuwa wakamilifu.


Na ikiwa wababa zetu wa kimwili walituadibisha, nasi tuliwaheshimu, jambo hilo halionyeshi zaidi kwamba tunapaswa kumuheshimu Baba yetu wa kiroho na kupata kuishi?


Halafu, mufalme Zedekia alimwapia Yeremia kwa siri akisema: Kama vile Yawe, yule aliyetupatia uzima, anavyoishi, sitakuua wala sitakutia katika mikono ya hawa wanaotaka kukuua.


Abrahamu akasema: “Nimesubutu kuzungumuza na Bwana, mimi ninayekuwa mavumbi na majivu tu.


Mbona haunisamehe kosa langu na kuniondolea uovu wangu? Hivi kisha muda kidogo nitalazwa chini katika mavumbi. Utanitafuta, lakini sitakuwa tena!


Yesu akalalamika kwa sauti kubwa akisema: “Baba, ninatoa uzima wangu kwako.” Kisha kusema maneno haya, akakata roho.


Walipokuwa wakimutupia mawe, Stefano akaomba akisema: “Ee Bwana Yesu, pokea roho yangu.”


Mungu anajua jinsi tulivyoumbwa; anajua kwamba sisi ni mavumbi.


Ukiwageuzia mugongo, wanaogopa; ukiondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi ndani ya mavumbi walimotoka.


Ninaweka roho yangu katika mikono yako; umenikomboa, ee Yawe, Mungu mwaminifu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite